Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwalimu, mkewe mbaroni kwa kumficha mtoto (8)
Habari Mchanganyiko

Mwalimu, mkewe mbaroni kwa kumficha mtoto (8)

Spread the love

JESHI la polisi mkoani Songwe linamshikilia Mwalimu Baraka Mwashihuya mkazi wa kitongoji cha Tazara – Mamlaka ya mji mdogo wa Mlowo wilayani Mbozi mkoani Songwe, pamoja na mkewe ambaye ni mwalimu wa sekondari ya Msense kwa tuhuma ya kumficha mtoto wa miaka nane chumbani. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe… (endelea).

Mwandishi wa habari hii Ibrahim Yassin (kulia), akimsalimia Mchungaji Korneli Mwasote ambaye ni baba wa mtoto aliyedaiwa kufichwa ndani kwenye nyumba ya Mwalimu Mwashihuya ambaye anashikiliwa na jeshi la polisi.

Akizungumza tukio hilo jana tarehe 31 Januari 2024, Bibi wa mtoto huyo, Sevelina Lwesye amesema tarehe 29 Januari mwaka huu mjukuu wake aitwaye Bradness Korneli Mwasote (8) hakuonekana nyumbani ndipo walipoanza kumtafuta pasipo mafanikio.

Amesema ilipofika jioni waliitaarifu serikali ya kijiji ambao waliungana nao kumtafuta pasipo mafanikio lakini walipata taarifa kwa msamaria mwema mmoja aliyewaonesha nyumba ya Mwalimu Mwashihuya.

Amesema baada ya kuoneshwa alipo mjukuu ndipo walipolitaarifu jeshi la polisi ambao walifika na kupekuwa chumba kimoja baada ya kingine na kumkuta mtoto huyo amefunikwa na blanketi mbili pamoja na godoro.

Amesema polisi walimtoa mtoto akiwa amedhoofu kutokana na njaa ya kutokula kwa siku nzima.

Baba wa mtoto huyo Korneli Mwasote ambaye ni mchungaji  wa kanisa la TAG Mbeya amesema alipatwa na mshangao juu ya tukio hilo lakini anamshukuru Mungu kwa kuwa mtoto wake amemkuta akiwa salama.

Katibu wa Mwenyekiti wa kitongoji cha Tazara, Smith Muyombe licha ya kuthibitisha uwepo wa tukio hilo, amesema hilo ni tukio la pili kutokea kwani mwishoni mwa mwaka jana alikamatwa mtu mmoja aliyeiba mtoto wa miezi minne.

Amesema mtu huyo alikamatwa na sasa yupo gerezani. Ameongeza na kutokana na hali hiyo zaidi wananchi 71 wamejiorodhesha wakitaka watuhumiwa wanaoiba watoto wahamishwe katika mtaa huo.

Kaimu kamanda wa polisi mkoani Songwe, Gallus Hyera licha ya kuthibitisha uwepo wa tukio hilo, amesema atalizungumzia kwa kina.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

error: Content is protected !!