Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msajili wa vyama aitwanga barua Chadema
Habari za Siasa

Msajili wa vyama aitwanga barua Chadema

Sisty Nyahoza, Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania
Spread the love

 

OFISI ya Msajili wa Vyama vya Siasa Tanzania, imekiandikia barua Chama Kikuu cha Upinzani nchini humo, Chadema, ikikitaka kijieleze juu ya kauli iliyotolewa na Katibu Mkuu wake, John Mnyika dhidi ya Rais Samia Suluhu Hassan. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa jana Alhamisi, tarehe 12 Agosti 2021 na Mnyika, katika ukurasa wake wa Twitter.

Kupitia mtandao huo, Mnyika amesema ofisi hiyo inakituhumu Chadema kwa kosa la kutumia lugha chafu dhidi ya Rais Samia.

Kauli hiyo chafu inadaiwa kutolewa na Mnyika, wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, tarehe 10 Agosti 2021, ambapo alidai Rais Samia alitoa kauli za uongo katika mahojiano yake na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).

“Msajili wa Vyama ameniletea barua tarehe 12 Agosti 2021, kutaka niwasilishe maelezo tarehe 13 Agosti 2021 kwa kusema kuwa Rais alitoa kauli za uongo kwenye mahojiano yake na @bbcswahili . Amedai kutumia maneno hayo ni lugha chafu, kashfa na kinyume na maadili,” imesema taarifa ya Mnyika.

MwanaHALISI Online imemtafuta kwa simu Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Sixty Nyahoza, kuhusu suala hilo, ambaye amejibu “Ndiyo tumeandika barua na tumewaisilisha.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!