Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mrithi wa Dk. Tulia kupatikana Februari 11
Habari za Siasa

Mrithi wa Dk. Tulia kupatikana Februari 11

Dk. Tulia Ackson, Spika wa Bunge la Tanzania
Spread the love

 

BUNGE la Tanzania limetanganza mchakato wa kujanza nafasi ya naibu spika wa Bunge ambapo uchaguzi wake utafanyika tarehe 11 Februari 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Uchaguzi huo unafanyika kujaza nafasi hiyo iliyoachwa wazi na Dk. Tulia Ackson ambaye alijiuzulu tarehe 31 Januari 2022, baada ya kuteuliwa na chama chake- Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwania uspika.

Dk. Tulia alikuwa miongoni mwa wagombea tisa waliojitokeza kugombea uspika Jumanne iliyopita ya tarehe 1 Februari 2022 na kushinda kwa kura zote za wabunge 376 waliopiga kura sawa na asilimia 100.

Dk. Tulia amechukua nafasi ya Job Ndugai ambaye tarehe 6 Januari 2022 alitangaza kujiuzulu.

Ndugai alichukua uamuzi huo baada ya kushinikizwa na viongozi wa CCM kutokana na kauli yake ya kukosoa mwenendo wa serikali kukoka fedha nje za kugharamikia miradi ya maendeleo kokosolewa vikali.

Leo Alhamisi, tarehe 3 Februari 2022, Ofisi ya Bunge imetoa taarifa kwa umma kikivitaarifu vyama vyenye uwakilishi bungeni kuweza kuanza mchakato wa kujaza nafasi hiyo.

“Chama kinachokusudia kushiriki uchaguzi, kinashauriwa kuanza mchakato wa kumpata mgombea kutoka miongoni mwa wabunge wa chama hicho,” imeeleza taaifa hiyo na kuongeza:

“Uchaguzi umepangwa kufanyika tarehe 11 Februari 2022. Hivyo jina la mgombea linapaswa kuwasilishwa kwa msimamizi wa uchaguzi kabla ya saa 10:00 jioni ya tarehe 10 Februari 2022, katika ofisi ya katibu wa Bunge.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!