Tuesday , 21 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mmoja wa pacha waliotenganishwa Muhimbili afariki
Habari MchanganyikoTangulizi

Mmoja wa pacha waliotenganishwa Muhimbili afariki

Spread the love

SIMANZI. Ndivyo unavyoweza kusema baada ya mmoja wa pacha waliotenganishwa Muhimbili, Neema kufariki dunia Jumapili tarehe 10 Julai, 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Neema amefariki dunia chini ya uangalizi maalumu ikiwa ni siku 10 tangu atenganishwe na pacha mwenzake Rehema tarehe Mosi Julai, 2022, upasuaji ambao ulielezwa kuwa na mafanikio makubwa licha ya changamoto kadhaa kutokana na namna walivyokuwa wameungana.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Hospitali hiyo, Aminiel Aligaesha na kueleza kuwa alifariki baada ya hali yake kubadilika badilika ghafla licha ya jitihada za madaktari.

“Nasikitika kukufahamisha kuwa mtoto Neema ambaye alitenganishwa na mwenzake Rehema amefariki jumapili ya tarehe 10 Julai saa 3 asubuhi,” amesema Aligaeshi katika taarifa yake hiyo na kuongeza;

“Akiwa ICU hali yake ilibadikika gafla, madaktari walijitahidi kurudisha hali yake bila mafanikio na hatimaye kupoteza maisha.

Taarifa hiyo haijaeleza kwa undani hali ya pacha mwingine aliyebakia zaidi ya kuleza kuwa bado yupo ICU na kutaka aendelee kuombewa.

“Twendelee kumwombea Rehema ambaye bado yupo ICU ili Mwenyezi Mungu amjalie afya njema,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Hukumu mahakama kuu yabatilishwa kesi State Oil, Equity Bank Tz

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imebatilisha hukumu iliyotolewa...

AfyaKimataifaTangulizi

Waliowekewa damu yenye VVU, homa ya ini kulipwa fidia trilioni 32.9

Spread the loveWaziri mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak ameahidi kulipa fidia ya...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yanawa mikono fidia Kimara-Kibamba

Spread the loveSERIKALI imewataka waathiriwa wa bomoabomoa ya upanuzi wa barabara ya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Geita, Mwanza waongoza kwa mbwa

Spread the loveNaibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Alexander Mnyeti amesema taarifa...

error: Content is protected !!