Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mipango ya Jaji Mutungi, Lipumba kumng’oa Maalimu Seif yafichuka
Habari za SiasaTangulizi

Mipango ya Jaji Mutungi, Lipumba kumng’oa Maalimu Seif yafichuka

Spread the love

KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad amesema kuwa Msajili wa vyama siasa nchini Jaji Francis Mutungi na Mwenyekiti anayetambuliwa na Ofisi yake Profesa Ibrahimu Lipumba wamepanga njama ya kukisambatisha chama hiko pamoja na kumfukuza Katibu mkuu huyo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Maalimu Seif ameyasema hayo leo alipokutana na wanachama wa chama hicho wa Tandale Jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa umesukwa mpango mahususi wa kung’oa ili kukisambaratisha chama hicho.

Amesema kuwa ziara ya Lipumba ya wiki iliyopita ilikuwa ni sehemu ya mpango huo uliosukwa na Msajili wa vyama vya siasa na kushirikiana na Balozi Seif Ali Iddi Makomo wa pili wa Rais Zanzibar ili kupatikane kwa wazanzibar wanaomuunga mkono Lipumba ili kupatikane uhalili wa kikatiba wa kuwa na wanachama Tanzania bara na visiwani ili kuweza kupora chama hicho.

Amesema kuwa Balozi Seif Ali Idd amekuwa mstari wa mbele kwenye mpango huo ili kuifukia haki ya wananchi wa Zanzibar ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Maalim Seif amesema kuwa Lipumba alipofika Zanzibar hakuna Mwanachama yoyote wa CUF aliyekwenda kumpokea Zaidi ya askari Polisi waliokuwa wakimlinda.

“Waliompokea ni askari waliovaa kiraia na wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na ADC”

Amesema ni wazi Lipumba hawezi kupata wafusi Zanzibar wa kuweza kukidhi matakwa yta kikatiba lakini Msajili Mutungi amemuahidi atampitisha hivyo hivyo.

“Msajili kashamwambia kuwa yeye atafute watu angalau 15 ili wapitishe …..Lipumba anafanya kazi na Seif ali Idd anyejita Makamo wa pili wa Rais anafanyakazi na Hamadi Rashidi …. Kwa lengo la kuisambratisha CUF Zanzibar.

“Wanajua kwa mazingira ya unguja na pemba kupata idadi ya kikatiba wanancha 5o haiwekani lakini wanaambizana kuwa nendeni kwa vile msajili amewaambia wajumbe 15 wanatosha”.amesema Maalimu Seif.

Maalimu Seif ameeleza kuwa Lipumba amekuwa akiinga Zanzibar kama mwizi na hukuitana na viongozi waandamizi wa CCM.

Maalimu seif amesititiza kutokuinga mkono Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambapo amesema kuwa serikali hiyo ni haramu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!