Wednesday , 27 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Lowassa, Mbowe waufuata waraka wa Maaskofu KKKT
Habari za SiasaTangulizi

Lowassa, Mbowe waufuata waraka wa Maaskofu KKKT

Spread the love

MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe na Mjumbe wa Kamati Kuu wa Chama hicho, Edward Lowassa wameshiriki kwenye ibada ya Jumapili ya matawi kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Azania Front,  Dar es Salaam. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Ujumbe waliotoka nao viongozi hao ni amani inayotakwenda sambamba na haki kwa pande zote.

Akizungumza nje ya Kanisa hilo baada ya ibada hiyo, Mbowe amesema kuwa viongozi wa dini wamehubiri amani na kusisitiza kutenda haki kutokana na kushabihiana kwa masuala hayo.

“Neno la leo ni amani na amani inapatikana kwa kutoa haki hivyo wachungaji wetu wamesema kuwa haki itendeke kwenye familia hadi kwa viongozi,” amesema Mbowe.

Mbowe amesema kuwa Pasaka ni Sikukuu muhimu kwa waumini wa dini ya kikristo  na ni siku inaazimisha kuteswa kufa, kuzikwa na kufufuka Yesu.

“Ni siku ambayo wakiristo tunaiona kuwa ni chanzo ukombozi na amani ya mwadamu ni chanzo cha kukoshwa kwa zambi zetu na damu ya kristo,” amesema Mbowe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!