MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe na Mjumbe wa Kamati Kuu wa Chama hicho, Edward Lowassa wameshiriki kwenye ibada ya Jumapili ya matawi kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Azania Front, Dar es Salaam. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Ujumbe waliotoka nao viongozi hao ni amani inayotakwenda sambamba na haki kwa pande zote.
Akizungumza nje ya Kanisa hilo baada ya ibada hiyo, Mbowe amesema kuwa viongozi wa dini wamehubiri amani na kusisitiza kutenda haki kutokana na kushabihiana kwa masuala hayo.
“Neno la leo ni amani na amani inapatikana kwa kutoa haki hivyo wachungaji wetu wamesema kuwa haki itendeke kwenye familia hadi kwa viongozi,” amesema Mbowe.
Mbowe amesema kuwa Pasaka ni Sikukuu muhimu kwa waumini wa dini ya kikristo na ni siku inaazimisha kuteswa kufa, kuzikwa na kufufuka Yesu.
“Ni siku ambayo wakiristo tunaiona kuwa ni chanzo ukombozi na amani ya mwadamu ni chanzo cha kukoshwa kwa zambi zetu na damu ya kristo,” amesema Mbowe.
Leave a comment