HALMASHAURI ya mji Tunduma wilayani Momba mkoani Songwe imetenga Sh 40 milioni kujenga stendi ya magari madogo zikiwemo daladala aina ya Hiace kwa fedha zake za mapato ya ndani ili kupunguza adha za usafirishaji mkoani Songwe. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).
Hayo yameelezwa jana Jumatatu na Mkurugenzi mtendaji wa mji Tunduma, Philimon Magesa katika kikao cha baraza la madiwani.
Amesema kutokana na uwepo wa stendi kuu Mpemba wameamua kujenga stendi ndogo iuli kupunguza msongamano kwenye stendi hiyo.
Amesema baada ya serikali kuwapatia fedha kujenga stedi kuu iliyopo kata ya Mpemba na halmashauri kutoa Sh 500 milioni za mapato ya ndani kujenga barabara ya kiwango cha lami eneo la kuzunguka soko, pia wametoa tena Sh 40 milioni kujenga stendi ya kugeuzia gari ndogo eneo la Chipaka.
“Stendi hiyo ni kwa ajili ya gari ndogo zikiwemo Hiace zinazotoka Mlowo hadi stendi ya Mpemba ili zikishusha abiria ziende hadi stendi ya Chipaka kushusha mizigo na kupakia abiria kisha kurudi stendi ya mpemba” amesema Magesa.
Naye Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Ayoub Mlimba amesema lengo la kujenga stendi hiyo ni kupunguza adha zilizopo kwani Tunduma ni mji wa kibiashara.
Amesema stendi hiyo itarahisisha abiria wakiwemo wafanyabiashara kupeleka bidhaa zao maeneo ya masoko yaliyopo Mjini.
Leave a comment