Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge aichongea Efatha Ministry bungeni kisa mauaji ya wananchi
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge aichongea Efatha Ministry bungeni kisa mauaji ya wananchi

Nabii Mwingira
Spread the love

MBUNGE wa Kwela, Deus Sangu, amewasilisha hoja ya dharura bungeni jijini Dodoma, akitaka kikao cha Bunge kiahirishwe kwa muda ili kujadili mgogoro sugu wa ardhi kati ya wananchi na mwekezaji wa shamba la Malonje, Efatha Ministry, baada ya kuibuka mauaji ya raia yanayodaiwa kufanywa na walinzi wa taasisi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Akiwasilisha hoja hiyo bungeni jijini Dodoma, leo tarehe 7 Novemba 2023, Sangu amedai licha ya Waziri wa Ardhi, Jerry Silaa, kuahidi kutembelea katika shamba hilo ili kutatua mgogoro tarehe 17 Novemba mwaka huu, jana tarehe 6 Novemba mwaka huu, mauaji hayo yametokea.

Sangu amedai kuwa, ameamua kuwasilisha hoja hiyo baada ya kulalamika bungeni zaidi ya mara tatu, lakini Serikali imeshindwa kuchukua hatua madhubuti, kitendo alichodai kuwa kinapelekea wananchi wa eneo husika kuendelea kunyanyasika.

Deus Sangu

Mbunge huyo wa Kwela, mkoani Rukwa, amedai walinzi wa Efatha Ministry jana waliwashambulia kwa risasi wananchi na kuwasababishia majeruhi huku baadhi yao wakipoteza maisha.

“Waziri wa Ardhi aliahidi atafika tarehe 17 Novemba 2023, lakini kabla hajafika limetokea tukio la ajabu sana, askari wanaolinda shamba hilo wamewapiga wananchi waliokuwa shambani risasi na kuwanyang’anya ng’ombe 42. Waliojeruhiwa ni Danson Charles aliyepigwa risasi ya tumboni na Festo Kamwanga, aliyepigwa risasi moja kifuani,” amedai Sangu.

Sangu amedai “haya yote nimeyaeleza lakini sijui nini kinachotokea, au kwa makusudi au kwa maslahi yaliyojificha hili jambo halijashughulikiwa. Hawa walinzi wamekuwa wakiwabaka kina mama hadi sasa 10 wamebakwa, wananchi walikatwa masikio,”

“Huyu mwekezaji ni nani ambaye anachukua mamlaka makubwa kutaka kuuwa watu? Wananchi wangapi wafe ndio Serikali ichukue hatua?”

Baada ya Sangu kuwasilisha hoja hiyo, Mwenyekiti wa Bunge, Daniel Sillo, aliitaka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, itoe ufafanuzi.

Naibu Waziri wa Ardhi, Geofrey Pinda, alikiri mauaji hayo kutokea huku akiahidi watafika eneo la tukio kwa ajili ya kumaliza mgogoro huo.

Kufuatia majibu hayo, Sillo aliitaka wizara hiyo ikifike haraka katika eneo la mgogoro huo kwa ajili ya kuchukua hatua.

“Niombe Serikali iende eneo la tukio haraka iwezekanavyo kwenda kuangalia hali ya majeruhi namna gani ya kuwasaidia kwa matibabu na kushiriki mazishi ya wengine waliopoteza maisha,” amesema Sillo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

Habari za SiasaTangulizi

Maafa Manyara: Rais Samia akatisha ziara yake Dubai

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amekatisha ziara yake...

Habari za SiasaTangulizi

Wataalaam wa miamba watua Hanang

Spread the loveWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na...

error: Content is protected !!