Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Mikoa sita yenye udumavu Tanzania yatajwa
Habari Mchanganyiko

Mikoa sita yenye udumavu Tanzania yatajwa

Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imetaja mikoa sita inayoongoza kwa tatizo la udumavu, kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mikoa hiyo inaongozwa na Njombe yenye asilimia 53.6 ya watoto wenye tatizo hilo, ikifuatiwa na Rukwa (47.9%), Iringa (47.1%), Songwe (43.3%), Kigoma (42.3%) na Ruvuma (41.0%)

Hayo yamesemwa leo Jumanne tarehe 19 Mei, 2020 na wizara ya kilimo wakati ikijibu swali la Dunstan Kitandula, Mbunge wa Mkinga (CCM), aliyehoji mkakati wa serikali katika kukabiliana na tatizo la utapiamlo nchini.

Katika swali lake ambalo limejibiwa kwa njia ya mtandao, Kitandula amesema utapiamlo ni janga kubwa nchini kwa kuwa kati ya watoto 100, watoto 30 wana tatizo la udumavu wa akili, huku kati ya watoto 100, watoto 59 wana tatizo la upungufu wa damu.

Kitandula amesema changamoto hiyo inasababisha Serikali kutumia fedha nyingi kukabiliana na tatizo hilo, ambazo zingeweza kutumika katika sehemu nyingine, kama kilimo kingeboreshwa ili kuwezesha upatikanaji wa mazao ya lishe bora.

Akijibu swali hilo, waziri wa kilimo amesema, wizara yake imeanza kutoa mafunzo ya uzalishaji, utayarishaji na ulaji wa vyakula vilivyoongezwa virutubishi katika mikoa yenye asilimia kubwa ya tatizo la udumavu kwa watoto.

“Mafunzo haya yanalenga kujengea uwezo wa jamii, katika kuzalisha na kutumia mazao yaliyoongezewa virutubishi kibaiyolojia, hatimaye kukabiliana na upungufu wa vitamini na madini mwilini hususan watoto,  chini ya miaka mitano na kina mama wajawazito na wanaonyonyesha,” amejibu.

Amesema wizara ya kilimo inashirikiana na wizara nane zinazohusika na masuala ya lishe nchini, kutekeleza mpango jumuishi wa kitaifa wa lishe, ili kutokomeza tatizo hilo.

“Aidha kwa kushirikiana na wizara ya viwanda na biashara, virutubishi vinaongezwa (Fortification) katika baadhi ya bidhaa zenye matumizi makubwa. Kwa mfano, madini chuma, Zinki na Vitamini B9 (Folic acid) huongezwa kwenye unga, ambapo Vitamini A huongezwa katika mafuta ya kupikia,” amesema Hasunga na kuongeza:

“Wizara pia, ina jukumu la kuelimisha jamii kuhusu uzalishaji wa mazao mchanganyiko (crop diversification) na matumizi ya vyakula vinavyotokana na mazao hayo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

Habari Mchanganyiko

Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Greyhorse zasaini mkataba wa bil.7.4

Spread the loveTAASISI ya Mwalimu Nyerere (MNF) imesaini mkataba wa miaka 10...

error: Content is protected !!