Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Meneja reli ya SGR abambwa akitorosha fedha
Habari Mchanganyiko

Meneja reli ya SGR abambwa akitorosha fedha

Dola za Marekani
Spread the love

YETKIN Gen Mehmen, Meneja Uwezeshaji wa Kampuni ya Yapi Merkezi, inayojenga mradi wa reli ya kisasa (SGR) nchini Tanzania, amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu ama kulipa faini ya Sh. 100 milioni pia kutaifishwa Dola za Marekani 84,850 alizokutwa nazo. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Leo tarehe 27 Februari 2020, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam imetoa hukumu hiyo baada ya kuthibitika, kwamba Yetkin alitaka kusafirisha fedha hizo nje ya nchi kinyume cha sheria.

Bosi huyo wa SGR ambaye ni raia wa Uturuki, alikutwa na ‘mzigo’ huo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), tarehe 13 Februari 2020.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hivyo, Yetkin amekiri kushindwa kufuata taratibu ikiwa ni pamoja na kushindwa kutoa maelezo kuhusu kitita cha fedha alichokutwa nacho JNIA.

Hakimu Simba amesema, kwa kuwa Yetkin amekiri kosa hilo, amehukumiwa kulipa faini ya Sh. 100 milion ama kwenda jela miaka mitatu ikiwa ni pamoja na kutaifishwa fedha hizo na kuwa mali ya Serikali ya Tanzania.

Shadrack Kimaro, Wakili wa Serikali Mkuu alimsomea mtuhumiwa huo mashtaka kwamba tarehe tajwa alikamatwa NJIA akiwa na begi la mkononi lenye kiasi hicho cha fedha na kwamba, alishindwa kutoa ufafanuzi kuhusu fedha hizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!