Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Chadema watolea uvivu wabunge wa CCM bungeni
Habari za Siasa

Mbunge Chadema watolea uvivu wabunge wa CCM bungeni

Aida Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

 

MBUNGE wa Nkasi Kaskazini, (Chadema), Aida Khenani, amewataka baadhi ya wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM), “waache unafiki” ili wamsaidie Rais Samia Suluhu Hassan, katika kufikia malengo yake ya kuliletea taifa maendeleo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Khenani ametoa wito huo leo tarehe 4 Aprili 2023, akichangia hoja ya ya azimio la Bunge kumpongeza Rais Samia kwa kuimarisha demokrasia na kukuza demokrasia ya uchumi, bungeni jijini Dodoma.

“Maridhiano yanayoendelea ni afya kwa taifa ili lifike uchumi tunaofikiri, ni lazima turuhusu mawazo mbadala maana utayapima kama yana maslahi kwa taifa utayatumia. Naunga mkono azimio hili endapo sisi Bunge tutamsaidia Rais, lakini tukikaa kwenye unafiki hatuamsaidia Rais,” amesema Khenani.

Akichangia azimio hilo la kumpongeza Rais Samia kwa kuimarisha demokrasia, Khenani amehoji wabunge wa CCM msimamo wao ni upi kwa kuwa kipindi mikutano ya hadhara inafungiwa walipiga makofi bungeni kupongeza hatua hiyo na sasa wanapiga makofi kumpongeza Rais Samia kwa kuifungua.

“Kuhusu kukuza demokrasia Napata mazingira magumu sana kwamba ni kweli amekuza demokrasia lakini amekuza demokrasia iliyodhohofishwa na nani na wa chama gani? Tunapozungumza mikutano ya hadhara yalizungumzwa hapa na Mwigulu kwamba lazima tutenge muda wa kufanya kazi na muda wa mikutano tulipiga makofi,” amesema Khenani.

Khenani amehoji “wabunge wa ndani ya Bunge hili leo tunapongeza kurudisha mikutano ni kweli tunapongeza kurudisha lakini nani aliondoa na wa chama gani? Sisi wabunge tunasimama wapi?”

Katika hatua nyingine, ameishauri mchakato wa marekebisho ya katiba uanze mara moja, ili kuenzi mambo mazuri yanayofanywa na Rais Samia hata kipindi ambacho ataondoka madarakani.

“Ili tufikie malengo ya maridhiano ambayo Rais ameongoza lazima kuwepo katiba mpya, Rais ameonyesha CCM mko tayari lazima mchakato huu uanze mara moja kusimamia yale anayozungumza ili atakapokuja Rais mwingine afuate misingi ambayo katiba mpya itakuwa imeweka,” amesema Khenani na kuongeza:

“Leo anapongezwa hapa, akija mwingine atakubali hiyo mikutano au ataondoa tena wakati iko kwa mujibu wa sheria? Lazima msingi inayowekwa leo kwenye utawala bora ije isimamiwe na yeyote atakaepata nafasi hiyo.,”

Mbunge wa Mafinga Mjini kupitia CCM, Cosato Chumi, amejibu hoja wa Khenani iliyohoji kubadilika kwa msimamo wao akisema hatua hiyo inatokana na mazingira kubadilika.

1 Comment

  • (xi) Mhe. WAZIRI Mkuu baada ya SERIKALI KUHAMIA DODOMA LINI VYOMBO VYA HABARI VYA ITV, EATV, TBC, AZAM TV, WASAFI TV, MWANANCHI VITAHAMIA DODOMA KWA LAZIMA.(TULIBUNI DSM HATUWEZI KUBUNI DODOMA)SWAHILI

    (xii) Dissertation (Confession Time):- Do high Unemployment Rate Influence Someone other Guys Creativity in solving PROBLEM, PRIDE, SOCIAL STATUS, WEALTH and Planning (TITANIC SOLVERS IN PARLIAMENT)?!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!