Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe aweka kambi Shinyanga
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe aweka kambi Shinyanga

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa
Spread the love

 

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, ameendelea na utekelezaji wa operesheni mpya ya chama hicho, iliyozinduliwa hivi karibuni ‘Operesheni Haki’, na sasa amepiga kambi mkoani Shinyanga. Anaripoti Mwandishi Wetu, Shinyanga…(endelea).

Leo Jumamosi tarehe 29 Mei 2021, Mbowe na ujumbe wake, wamewasili mkoani Shinyanga, wakitokea jijini Arusha, baada ya kuzindua operesheni hiyo Alhamisi tarehe 27 Mei mwaka huu.

Katika ziara yake hiyo, Mbowe ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi ya Chadema, Wilaya ya Shinyanga Mjini.

Freeman Mbowe, Mwenyekiti Chadema Taifa

Katika hafla hiyo, Mbowe amewahakikishia wanachama wa Chadema mkoani Shinyanga, kwamba, atahakikisha anatafuta fedha za kukamilisha ujenzi huo, kabla ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024.

Pia, Mbowe amesema Chadema kitaendelea kujenga ofisi zake, katika kanda na mikoa mbalimbali, kwa kuwa chama hicho kinazidi kukua.

“Chama chetu kinaendelea kukua siku hadi siku, Shinyanga hatukuwa na makao makuu ya wilaya bali tumenunua jengo la kanda. Tutaendelea kujenga ofisi hizi kwa kushirikiana na wanachama, tuachangia kwa kuhakikisha linakamilika kabla ya uchaguzi ujao wa 2024 na 2025,” amesema Mbowe.

Mbali na uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi hiyo, Mbowe ataongoza kikao cha Kamati ya Utendaji ya Chadema ya Kanda ya Serengeti, katika ofisi za kanda hiyo zilizoko Shinyanga.

Operesheni Haki inatarajiwa kufanyika kwa muda wa mwezi mmoja na nusu kuanzia siku ilipozinduliwa, ambapo kwa kaunzia, itafanyika katika kanda zote 10 za Chadema, Tanzania Bara na Zanzibar, kisha itashushwa hadi ngazi ya chini.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!