Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Michezo Manchester United kuivaa AC Milani, 16 bora Europa
Michezo

Manchester United kuivaa AC Milani, 16 bora Europa

Spread the love

 

KLABU ya Manchester United itavaana na AC Milan kwenye hatua ya 16 ya michuano ya Kombe la Europa baada ya kuchezeshwa kwa droo mchana wa leo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwenye mchezo wa kwanza Manchester United ataanzia nyumbani kwenye Uwanja wa Old Trafford kwa kuikalika AC Milan mchezo utakaopigwa tarehe 11 Machi 2021, na marudiano yatapigwa 18 Machi 2021, jijini Milan nchini Italia.

Timu hizo zimekutana mara 10 kwenye michezo ya kimashindano huku Manchester United ikifanikiwa kushinda michezo mitano na AC Milan ikishinda michezo mitano huku kukiwa hamna sare hata moja.

Mara ya mwisho timu hizo zilikutana kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya tarehe 10 Machi 2010, Old Trafford na Manchester United ikafanikiwa kuondoka na ushindi wa mabao 4-0.

Michezo mingine ya Europa Ligi itakayopigwa tarehe 11 Machi 2021 ni Ajax dhidi ya Young Boys, Dynamo Kyiv watawaalika Vilarreal, Roma dhidi ya Shakhtar Donestsk, Olympiacos kuikabiri Arsenal.

Pia Dinamo Zagreb wataikabili Totenham, Slavia Praha dhidi ya Rangers na Granada akiwa nyumbani ataikabiri Molde.  

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Tusua kijanja na mechi za Europa leo

Spread the love  Alhamisi ya leo EUROPA inaendelea ambapo ni mechi za...

Michezo

Hapa Diego Simeone, pale Simeone Inzaghi kivumbi cha Ligi ya Mabingwa Ulaya

Spread the love LIGI ya Mabingwa ulaya itaendelea usiku wa leo ambapoitakwenda...

error: Content is protected !!