Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Manchester United kuivaa AC Milani, 16 bora Europa
Michezo

Manchester United kuivaa AC Milani, 16 bora Europa

Spread the love

 

KLABU ya Manchester United itavaana na AC Milan kwenye hatua ya 16 ya michuano ya Kombe la Europa baada ya kuchezeshwa kwa droo mchana wa leo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwenye mchezo wa kwanza Manchester United ataanzia nyumbani kwenye Uwanja wa Old Trafford kwa kuikalika AC Milan mchezo utakaopigwa tarehe 11 Machi 2021, na marudiano yatapigwa 18 Machi 2021, jijini Milan nchini Italia.

Timu hizo zimekutana mara 10 kwenye michezo ya kimashindano huku Manchester United ikifanikiwa kushinda michezo mitano na AC Milan ikishinda michezo mitano huku kukiwa hamna sare hata moja.

Mara ya mwisho timu hizo zilikutana kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya tarehe 10 Machi 2010, Old Trafford na Manchester United ikafanikiwa kuondoka na ushindi wa mabao 4-0.

Michezo mingine ya Europa Ligi itakayopigwa tarehe 11 Machi 2021 ni Ajax dhidi ya Young Boys, Dynamo Kyiv watawaalika Vilarreal, Roma dhidi ya Shakhtar Donestsk, Olympiacos kuikabiri Arsenal.

Pia Dinamo Zagreb wataikabili Totenham, Slavia Praha dhidi ya Rangers na Granada akiwa nyumbani ataikabiri Molde.  

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!