Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko IGP Sirro: Hatufungui kesi za madai, migogoro ya ardhi
Habari Mchanganyiko

IGP Sirro: Hatufungui kesi za madai, migogoro ya ardhi

Spread the love

 

INSPEKETA wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania, Simon Sirro ameema, ili kupunguza mrundikano wa mahabusu vituoni, hawafungia kesi za madai na migogoro ya ardhi na jukumu hilo sasa linafanywa na mahakama. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

IGP Sirro amesema hayo leo Ijumaa tarehe 26 Februari 2021, mbele ya Rais John Magufuli, aliyefungua jiwe la msingi la ujenzi wa Kiwanda cha Ushonaji katika Bohari Kuu ya Jeshi la Polisi.

Pia, Rais Magufuli amezindua majengo ya ofisi, madarasa pamoja na bweni la wanafunzi, Chuo cha Taaluma ya Polisi, Dar es Salaam.

“Hatutaruhusu kufungua kesi za madai polisi, kesi za madai ziende moja kwa moja mahakamani na zile za migogoro ya ardhi na kufanya hivi mheshimiwa Rais, imepunguza mrundikano wa mahabusu,” amesema IGP Sirro.

Kuhusu suala la upepezi, IGP Sirro amesema “sisi tumejipanga kuhakikisha upelelezi wa kesi mbalimbali unamalizika mapema, kesi ndogondogo zinakwisha ndani ya miezi sita na kesi kubwa zinamalizika ndani ya mwaka mmoja.”

Inspekta huyo wa polisi, ametoa onyo kwa wahalifu hususan wanaotumia silaha akisema “awamu hii si ya kuendekeza matumizi ya silaha au ugaidi. Wale ambao hawataki kubadilika, tutawabadilisha na mtu akichukua bunduki yake nyumbani, aage kabisa kwani hatuna muhali na hili.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!