Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mamia wamuaga kaka yake Mbowe
Habari Mchanganyiko

Mamia wamuaga kaka yake Mbowe

Spread the love

MAMIA ya watu leo tarehe 2 Agosti 2019, wamejitokeza katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Nshara Machame kuuagwa mwili wa Meja Jenerali mstaafu, Alfred Mbowe. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Alfred ni kaka wa Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), mazishi yake yanatarajiwa kufanyika katika Kijiji cha Nshara, Hai mkoani humo.

Meja huyo alifariki dunia tarehe 28 Julai 2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambapo aliagwa jijini Dar es Salaam tarehe 31 Julai 2019.

Viongozi mbalimbali wa dini, wameshiriki ibada hiyo ambapo jijini Dar es Salaam, Rais John Magufuli, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na viongozi wengine walipata fursa ya kuuaga mwili wa Alfred (66). Alistaafu jeshi mwaka 2009.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!