Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mambo 6 kutikisa vikao Kamati za Bunge
Habari za Siasa

Mambo 6 kutikisa vikao Kamati za Bunge

Spread the love

MAMBO sita yanatarajiwa kutikisa katika vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania vitakavyoanza Januari 19 hadi 29 mwaka huu, ikiwemo kupokea na kujadili taarifa mbalimbali za utekelezaji wa maazimio ya Bunge. Anaripoti Jonas Mushi…(endelea)

Kamti hizo zinakutana kabla ya Mkutano wa 10 wa Bunge uliopangwa kuanza tarehe 31, Januari, 2023.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Alhamisi tarehe 5 Januari, 2023 na Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa Ofisi ya Bunge, shughuli zilizopangwa kufanywa na Kamati katika vikao hivyo ni pamoja na kupokea na kujadili Taarifa za Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge yaliyotokana na Taarifa za Mwaka za Shughuli za Kamati zilizowasilishwa bungeni Februari, 2022.

Taarifa hiyo pia imeeleza kuwa kamati zitapokea na kujadili taarifa mbalimbali kuhusu shughuli za Umma nchini ili kufuatilia utekelezaji wa sera na mipango ya sekta zinazohusika.

Pia kamati mbili zinazohusika na kusimamia matumizi ya fedha za umma yaani Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) na Kamti ya Hesabu za Seriklai za Mitaa (LAAC), zitakuwa na kibarua cha kuchambua taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  kuhusu kaguzi Maalumu na Kaguzi za Ufanisi.

Kazi nyingine itakayofanywa katika kipindi hicho ni kupokea na kchambua taarifa ya uwekezaji wa mitaji ya umma ili kubaini iwapo uwekezaji huo una ufanisi na kuwa umezingatia taratibu, sheria na miongozo mujarabu ya biashara.

Pia kamati zitapokea na kujadili Taarifa kutoka kwenye Wizara na Taasisi mbalimbali kuhusu ukusanyaji wa mapato, usimamizi wa vyanzo vya mapato na utekelezaji wa bajeti.

Aidha Kamati ya Sheria Ndogo itachambua sheria ndogo zilizowasilishwa wakati wa Mkutano wa Tisa wa Bunge sambamba na kupokea na kuchambua taarifa ya utekelezaji wa Maazimio ya Bunge kuhusu Sheria Ndogo ziilizowasilishwa katika Mkutano wa Tano, Sita na Saba wa Bunge.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo kamati mbili zinatarajiwa kuanza shughuli zake mapema zaidi tarehe 9 Januari ikiwemo Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Makamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!