Sunday , 12 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Makamba akabidhiwa Ofisi, apewa zigo la diplomasia ya uchumi
Habari Mchanganyiko

Makamba akabidhiwa Ofisi, apewa zigo la diplomasia ya uchumi

Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amekabidhiwa ofisi rasmi na aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo, Dk. Stergomena Tax katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Waziri Makamba amemshukuru Dk. Tax kwa ushirikiano aliompatia wakati wote tangu yalipofanyika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri mwishoni mwa mwezi Agosti 2023.

“Tangu Mheshimiwa Rais alipofanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri umekuwa ukinipatia ushirikiano wakati wote, nakushukuru sana, pia nakutakia heri katika majukumu yako mapya” amesema Waziri Makamba

Naye Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Tax amesema alipohudumu katika Wizara hiyo alipata ushirikiano mkubwa kutoka kwa menejimenti na watumishi wa Wizara na kumhakikishia Waziri Makamba kuwa ana watumishi wachapakazi

“Wakati wa utumishi wangu hapa wizarani, nilipata ushirikiano mkubwa, hivyo napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru sana menejimenti na watumishi wote wa wizara kwa ushirikiano walionipa,” alisema Dk. Tax

Amesema jukumu lililo mbele ya Wizara hiyo ni kutekeleza maono ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kutekeleza diplomasia ya uchumi kwa vitendo kwa kutafuta fursa mbalimbali za kukuza uchumi na kuendeleza diplomasia ya uchumi

Pamoja na mambo mengine, Dk. Tax pia amemtakia utendaji kazi mwema Waziri Makamba na kuwashukuru Naibu Waziri Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, Katibu Mkuu Mkuu wa Wizara, Balozi Dk. Samwel Shelukindo, Naibu Katibu Mkuu, Menejimenti na watumishi wa Wizara.

Makabidhiano hayo yalihudhuriwa pia na wajumbe wa menejimenti na baadhi ya watumishi wa wizara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

BiasharaHabari Mchanganyiko

PPAA yajipanga kuwanoa wazabuni namna kuwasilisha rufaa kieletroniki

Spread the loveIli kukabiliana na mageuzi yaliyofanyika katika Sheria mpya ya Ununuzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!