Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Majina waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza haya hapa
ElimuHabari Mchanganyiko

Majina waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza haya hapa

Wanafunzi wa darasa la saba wakifanya mtihani
Spread the love

BARAZA la Mitihani nchini (NECTA), limetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza nchini. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Akitangaza majina hayo leo tarehe 5 Desemba 2019, Selemani Jafo, Waziri wa Ncho, Ofisi ya Rais –Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) amesema, asilimia 92.27 ya wanafunzi waliofanya mtihani wa Darasa la Saba mwaka huu, wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza mwakani.

Amesema, asilimia hiyo inaakisi jumla ya wanafunzi 701,038 kwamba ndio waliochaguliwa.

Amesema, wanafunzi 58,699 wameshindwa kuchaguliwa kutokana na kukosa madarasa huku Mkoa wa Kigoma, ukiwa na kiwango kikubwa cha upungufu huo. Wanafunzi 909 ndio waliofutiwa matokeo kutokana na udanganyifu.

Amesema, katika wale waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza, wavulana ni 335, 513 na wasichana ni 365, 525.

Angalia majina ya wanafunzi wa darasa la saba na shule wanazoenda hapa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!