NANI alikuambia wameachana? Hawajaachana ng’o! ndivyo walivyowathibitishia mashabiki wao wasanii wa Bongofleva, Faustina Mfinanga ‘Nandy’ na William Lyimo ‘Billnass’ waliposhusha shoo kali katika kilele cha tamasha la ‘Nandy Festival’ jijini Dar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Wawili hao ambao kwa tangu Februari hawajaonekana hadharani pamoja, waliwafurahisha mashabiki baada ya kuperfom pamoja jana tarehe 4 Septemba 2021 katika shoo hiyo iliyopigwa katika viwanja vya Posta Kijitonyama.
Mauno ya Nandy, pamoja na mahaba murua ndiyo yaliyoinua shangwe za mashabiki hao ambao walipigia mstari kuwa couple hiyo imerudi upya.
Aidha, baada ya shoo hiyo, Billnass alimpa mashavu ya kutosha Nandy mbele ya waandishi wa habari kwa kueleza kuwa ni mwanamke imara ambaye ni mfano wa kuigwa kwa mabinti wanaotaka kuwa kama yeye kwenye kiwanda cha muziki.
“Kuhusu kufanya shoo pamoja ni kwamba watu wamekuwa wakipenda tupande jukwani pamoja ila bahati mbaya ratiba zangu zikawa zinanibana ila leo (jana) imewezekana kwa sababu naheshimu vitu anavyofanya… hii ni shoo, haihusiani na mapenzi,” alijidai Billnass.
Leave a comment