Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mabalozi nao kuhamishiwa Dodoma
Habari za Siasa

Mabalozi nao kuhamishiwa Dodoma

Spread the love

JUMLA ya Mabalozi 63 wameshakabidhiwa maeneo ya kujenga ofisi zao Katika Jiji la Dodoma lakini Ubalozi wa Zambia tayari umeshaanza mchakato huo kwa kuanza ujenzi wa nyumba ya Mkandarasi wake. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Kauli hiyo ilitolewa juzi na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi wakati akitambulisha mpango wa maonyesho ya wajenzi katika mkakati wa ‘Tunajenga Dodoma.’

Kunambi amesema mabalozi hao walikwenda wiki mbili zilizopita lakini juzi balozi wa Zambia akamuomba kumpatia kiwanja cha kununua haraka kwa ajili ya kujenga nyumba ya mkandarasi atakayekuwa akisimamia jengo la ubalozi.

Amesema mkakati umewekwa kwa ajili ya kuijenga Dodoma mpya itakayolingana na miji ya Abuja (Nigeia), Pretoria (Afrika ya Kusini) au Mji wa Nairobi nchini Kenya na kwamba Serikali imekwishatoa kiasi cha Sh 1.2 bilioni kwa ajili ya mapitio ya ramani ambayo hata hivyo hayataruhusu nyumba za watu kubomolewa isipokuwa kama kuna umuhimu zaidi.

Akizungumzia kuhusu vifaa vya ujenzi kwamba havitoshelezi, Meneja wa Tawi wa mabati ya Alaf Grayson Mwakasege, amesema dhata kuwa vifaa vya ujenzi kwa Dodoma ni vichache si ya kweli na kuwa imepitwa na wakati kwani bidhaa ipo ya kutosha isipokuwa watu wanatumia mwanya huo kutaka kuhalalisha manunuzi nje ya mkoa.

Mwakasege amesema ujenzi wa jiji hilo jipya hauwezi kumaliza malighafi iliyopo ambayo kila soko linavyopanuka ndivyo ambavyo wafanyabiashara wanavyoendelea kuongeza mitaji yao na kupeleka bidhaa hitajika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!