Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mabalozi mtegoni, Samia akerwa balozi aliyekataliwa kwa ugoigoi
Habari za SiasaTangulizi

Mabalozi mtegoni, Samia akerwa balozi aliyekataliwa kwa ugoigoi

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amewataka mabalozi wapya aliowaapisha leo Jumatano kuelekea kwenye vituo vyao vya kazi wakiwa wamekamilika kwa sababu muda wowote wanaweza ‘kutumbuliwa’ baada ya kupokea ripoti ya tathmini ya utendaji kazi wa wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki. Anaripoti Mlelwa Kiwale (TURDACo)…(endelea).

Pia ameeleza kukerwa na mabalozi wasiojielewa kwa kuendekeza uvivu huku baadhi yao wakifanya kazi ya kupokea ujumbe wa wageni kutoka Tanzania, kuwapangia ratiba na kushughulikia watanzania wakorofi katika nchi wanazowakilisha.

Rais Samia ametoa maagizo hayo leo tarehe 16 Agosti 2023 Ikulu Chamwino jijini Dodoma wakati akihutubia katika hafla ya kuwaapisha mabalozi wapya aliowapangia vituo vya kazi wiki iliyopita.

Baadhi ya mabalozi waliopishwa leo Ikulu Chamwino jijini Dodoma wakimsikiliza Rais Samia Suluhu Hassan

Amesema hivi karibu aliunda kamati maalumu ya kufanya tathmini kuhusu utendaji kazi wa wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki ambayo imempelekea ripoti ya awali kuhusu kasoro na maboresho ya wizara hiyo.

Amesema baada ya kupokea ripoti hiyo, ameirejeshea kamati hiyo na kuitaka kuiboresha hivyo atakapopokea ripoti kamili muda wowote mabalozi hata hao wapya waliopishwa leo wanaweza kurejeshwa nyumbani au kuhamishwa.

“Baada ya kupata ripoti ya kamati mnaweza mkageuzwa tena, nenda jiaminishe nimewekwa hapa naanza kazi kiukwelikweli, hatutegemei sana mabadiliko lakini yanaweza kutokea,” amesema.

Aidha, ameeleza kukerwa na baadhi ya mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi walizopangiwa kwenda kustarehe na familia zao badala ya kufanya kazi zilizowapekeleka.

Ametoa mfano kuwa Rais mmoja wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), alimuomba balozi wa Tanzania arejeshwe kwa kuwa goigoi (mvivu) hashiriki hata mikutano inayofanyika katika nchi hiyo.

“Katika nchi nyingine mabalozi wetu hawajui wanachokifanya… wapo tu, nilishakutana na rais mwenzangu ndani ya SADC akaniambia ‘nibadilishie balozi uliyeniletea, maana hata kazini haendi, mikutano hashiriki yupoyupo tu hatumuelewi kwa sababu Watanzania hatuwajazoea hivyo labda ubadilishe’, nikamuambia nimekusikia” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!