Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif: Vijana wapo tayari
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif: Vijana wapo tayari

Maalim Seif Sharif Hamad, aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
Spread the love

MAALIM Seif Shariff Hamad, mgombea urais visiwani Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, amesema safari hii vijana wapo tayari. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

“Tunapambana na CCM (Chama Cha Mapinduzi) na nafikiri vijana wengi safari hii wamejipanga na kujiandaa, likitokea lolote wapo tayari,” amesema Maalim Seif wakati akizungumza na gazeti moja la kila wiki, mapema wiki hii.

Akizungumzia ushindani uliopo kati yake na CCM, amesema ndani ya chama hicho, wapo wanaomuunga mkono kutokana na kutoridhishwa na mgombea aliyeteuliwa na chama hicho.

Mgombea aliyeteuliwa na CCM kugombea urais Zanzibar NI Dk. Hussein Ali Mwinyi na kwamba, anajua hapambani na Dk. Mwinyi pekee bali CCM wote.

“Tofauti iliyopo baina ya chaguzi zote hizo ni ndogo sana, kwa sababu chaguzi zote hizi tunashindana na wagombea wa CCM. na CCM ni ile ile na kwa kweli unaposhindana na CCM hushindani na mgombea, unashindana na CCM wote.

“…tofauti iliyopo  kubwa hivi sasa ndani ya CCM , hakuna ule umoja ambao walikuwa nao zamani. Watu wengi sasa hivi hawaridhishi na mgombea aliyeletwa na chama chao kuwania nafasi hiyo,” amesema Maalim Seif.

kwa hiyo, kidogo inatufanya tuamini kwamba kuna watu wengi wanaotuunga mkono ndani ya CCM.

Akizungumzia kauli ya kwamba yeye ni ‘mgombea mzoefu wa kushindwa’ amesema yeye si mzoefu wa kushindwa bali mzoefu wa kudanganywa.

“…sidhani kama mimi ni mzoefu wa kushindwa, lakini mimi ni mzoefu wa kudanganywa, kuanzia mwaka 1995, 2000, 2005, 2010 na hata 2015 nimekuwa nikishinda na ushahidi kamili ulipatikana mwaka 2015.

“Na hii kila mmoja alijua kama tumeshinda tena kwa kura nyingi sana, lakini mwenyekiti wa tume akapata maagizo ya kuwa afute uchaguzi kinyume cha Katiba na sheria, kwa hiyo kwamba nashindwa aaaah! nanyang’anywa,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!