Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mkakati wa Kubenea TFF huu hapa
Habari za Siasa

Mkakati wa Kubenea TFF huu hapa

Spread the love

SAED Kubenea, mgombea ubunge Kinondoni, jijini Dar es Salaam  kupitia Chama cha ACT-Wazalendo amesema, miongoni mwa mambo atakayosimamia ni kuhakikisha linaundwa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF), lisilokuwa na viongozi mashabikiwa wa vilabu vikubwa vya mpira nchini.  Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Amesema, shirika hilo ambalo litaundwa kwa mijibu wa Bunge, litasimamia michezo kwa haki na usawa.

Ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mzimuni iliyopo ndani ya jimbo hilo, wakati akiendelea na kampeni zake za mtaa kwa mtaa.

“Ukiwa na chama cha soka kinachosimamia michezo, ndani yake mkileta ushabiki wa Yanga na Simba, mpira hautaendelea. Tunataka watu ambao wakifika TFF, Simba na Yanga waziache nyumbani kwao, pale wakasimamie timu zote kwa kuwa wao ndio wasimamizi wa mpira wetu,” amesema Kubenea.

Walace Karia, Rais wa TFF

Pia ameahidi wananchi wa Kinondoni kwambwa, atahakikisha anawapa mikopo wafanyabiashara, kupunguza kodi na huku wafanyabiashara ndogondogo hawalipi kodi kubwa hadi wanapokuwa na kiwango cha wafanyabiashara wa kati.

Amesema, ana mpango wa kanzisha shule za sekondari za kidato cha tano na sita ndani ya jimbo hilo kwa kuwa, hazipo kwa sasa.”Tunataka kuimarisha vituo vya afya na hospitali za umma, kuhakikisha dawa zinapatikana na mtu aliyetimiza miaka 60 anahudumiwa bure.

“Tunataka mtu akifa katika hospitali ya serikali, mwili wa marehemu usizuiwe kwenda kuzikwa mpaka ulipiwe bili, aliyefiwa alipe akazike ndugu yake,” amesema.

Kubenea anaendelea kufanya kampeni za mtaa kwa mtaa katika maeneo mbalimbali ya jimbo hilo ikiwa ni pamoja na kuwatembelea waliokumbwa na maafa ya mafuriko kwenye Bonde la Mto Msimbazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!