Wednesday , 27 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif mguu nje, mguu ndani CUF
Habari za Siasa

Maalim Seif mguu nje, mguu ndani CUF

Spread the love

TAMKO la Maalim Seif Shariff Hamad, Katibu Mkuu wa CUF kwamba ‘muda ukifika nitazungumza’ kuhusu kuhama chama hicho inatikisa msimamo wake wa awali. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Tamko hilo amelitoa ikiwa ni siku nne baada ya kupata ‘mwaliko’ wa kujiunga na Chadema ambapo ameahidiwa kugombea nafasi ya urais visiwani Zanzibar kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020.

Ahadi hiyo ya Chadema ilitolewa na Hashim Juma, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Chadema.

Maalim Seif amesema kwamba, kwa sasa hawezi kuzungumzia suala la kwenda Chadema kwa sasa na kwamba, wakati ukifika atazungumza na waandishi.

Kauli ya Maalim Seif iliwasilishwa na Nassor Ahmad Mazrui, Naibu Katibu Mkuu wa CUF-Zanzibar

Kauli hiyo ya Maalim Seif inaonesha kulegeza msimamo wake wa awali kwamba hawezi kuhama CUF.

Msimamo huo unafanana na ule wa Ally Saleh, Mbunge wa Malindi (CUF) kwamba, wakati ukigika watajua wafanye nini ili wabaki kwenye Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Tayari Magdalena Sakaya, Naibu Katibu Mkuu CUF Bara amemtahadharisha Maalim Seif kwamba, akihama CUF itakuwa ndio mwisho wake wa siasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!