Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif mguu nje, mguu ndani CUF
Habari za Siasa

Maalim Seif mguu nje, mguu ndani CUF

Spread the love

TAMKO la Maalim Seif Shariff Hamad, Katibu Mkuu wa CUF kwamba ‘muda ukifika nitazungumza’ kuhusu kuhama chama hicho inatikisa msimamo wake wa awali. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Tamko hilo amelitoa ikiwa ni siku nne baada ya kupata ‘mwaliko’ wa kujiunga na Chadema ambapo ameahidiwa kugombea nafasi ya urais visiwani Zanzibar kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020.

Ahadi hiyo ya Chadema ilitolewa na Hashim Juma, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Chadema.

Maalim Seif amesema kwamba, kwa sasa hawezi kuzungumzia suala la kwenda Chadema kwa sasa na kwamba, wakati ukifika atazungumza na waandishi.

Kauli ya Maalim Seif iliwasilishwa na Nassor Ahmad Mazrui, Naibu Katibu Mkuu wa CUF-Zanzibar

Kauli hiyo ya Maalim Seif inaonesha kulegeza msimamo wake wa awali kwamba hawezi kuhama CUF.

Msimamo huo unafanana na ule wa Ally Saleh, Mbunge wa Malindi (CUF) kwamba, wakati ukigika watajua wafanye nini ili wabaki kwenye Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Tayari Magdalena Sakaya, Naibu Katibu Mkuu CUF Bara amemtahadharisha Maalim Seif kwamba, akihama CUF itakuwa ndio mwisho wake wa siasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!