Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Maalim Seif, majimbo 34 tunachukua Z’bar’
Habari za Siasa

‘Maalim Seif, majimbo 34 tunachukua Z’bar’

Maalim Seif Sharrif Hamad, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad atashinda urais wa Zanzibar na tuna uhakika wa kushinda majimbo 34 ya uchaguzi visiwani humo. Anaripoti Faki Sosi, Kigoma … (endelea).

Hiyo ni kauli ya Zitto Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo aliyoitoa tarehe 8 Julai 2020, mbele ya wanachama wa chama hicho Kigoma.

Zitto ameanza ziara yake kwenye Mikoa ya Magharibi, akianzia Kasulu ambapo amefanya vikao vya ndani na kukutana na viongizi wa ngazi mbalimbali pia wanachama wa chama hicho.

“Kule Zanzibar tunashinda majimbo 34, mapema asubuhi Maalim Seif rais Zanzibar, wamezoea kuiba, sasa Maalim Seif yupo chama cha ACT-Wazalendo, waibe waone.

“Tumeimarisha nguvu, uimara ujasiri wa Maalim Seif Hamad unakutana na nguvu ya kijana wenu Zitto kabwe,” Zitto amewaambia wanachama wa chama hicho Kigoma.

Maalim Seif mara kadhaa amenukuliwa akisema, safari hii hana uwezo wa kuwazuia Wazanzibari kupigania haki yao endapo ataporwa ushindi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!