Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Isaya Mwita: Aliyeng’olewa Umeya wa Jiji, ageukia urais
Habari za Siasa

Isaya Mwita: Aliyeng’olewa Umeya wa Jiji, ageukia urais

Mwita Isaya, aliyekuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam akikabidhiwa fomu ya kugombea Urais katika Uchaguzi Mkuu 2020 kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

MIEZI sita baada ya kung’olewa Umeya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Isaya amejitokeza leo kwenye ofisi za chama hicho zilizopo Mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es Salaam, na kukabidhiwa fomu hiyo na Reginald Munisi, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa chama hicho.

Isaya alitangazwa kuvuliwa umeya tarehe 9 Januari 2020, kwa madai mbalimbali.

Miongoni mwa tuhuma zake ni pamoja na kushindwa kuongoza kikao cha baraza la madiwani na kupendelea baadhi ya mameya kuingia katika kamati za fedha.

Alituhumiwa kuwa na matumizi mabaya ya gari umma kwa kulisababishia kupata ajali, jambo ambalo meya amekuwa akijibu kwamba yeye siyo dereva wa gari hilo.

Lakini pia kutotumia kiasi cha Sh. 5.8 bilioni, zilizotokana na mauzo ya hisa za Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), ambalo lilikuwa mali ya jiji.

Mwita Isaya, aliyekuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam akionyesha fomu ya kugombea Urais katika Uchaguzi Mkuu 2020 kwa tiketi ya Chadema

Isaya amechukua fomu leo tarehe 9 Julai 2020, Makao Makuu ya Chadema, Mtaa wa Ufipa jijini Dar es Salaam.

Mara baada ya kuchukua fomu hiyo, Isaya amesema kitu cha kwanza kwenye utawala wake ni Katiba Mpya kwa manufaa ya Watanzania wote.

“Katiba Mpya ndio jambo la kwanza nitakaloanza nalo endapo chama changu kitaniamini na kunipitisha na hatimaye kuwa Rais wa Tanzania, Katiba itaheshimiwa na kila mtu” amesema Isaya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!