Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif atoa sharti kukubali kushindwa Z’bar
Habari za Siasa

Maalim Seif atoa sharti kukubali kushindwa Z’bar

Maalim Seif Sharif Hamad, aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
Spread the love

MGOMBEA urais Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad amesema, ili akubali kushindwa katika uchaguzi mkuu utakaofanyika tarehe 27 na 28 Oktoba 2020, lazima uchaguzi huo uwe huru na haki. Anaripoti Mwandishi Wetu, …(endelea).

Akizungumza na kituo cha habari cha Uingereza (BBC), jana Jumatano tarehe 21 Oktoba 2020, Maalim Seif amesema, ikiwa uchaguzi huo utakuwa huru na haki, atampongeza mshindani wake Dk. Hussein Ali Mwinyi, mgombea kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Kama uchaguzi utakuwa huru na haki, sina tatizo, nitampongeza Dk. Hussein Mwinyi,” amesema Maalim Seif ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho Taifa.

Nguli huyo wa siasa za upinzani Zanzibar, tayari amewaweka wafuasi wa chama chake tayari kwa ajili ya kile alichosema ‘kutetea haki yao,’ iwapo itapokwa baada ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kutangaza matokeo ya uchaguzi huo mkuu.

Tarehe 20 Oktoba 2020, Maalim Seif alipozunguma na waandishi wa habari alisema, tofauti na chaguzi zilizopita, uchaguzi wa safari hii hatomzuia mtu yeyote kujitokeza na kutetea haki yake.

“Siku zote tulikuwa tukitahadharisha kwa kudhani kwamba wenzetu ni waungwana. Kwamba wenzetu watatilia maanani tunayozungumza, na siku zote mimi niseme, nilikuwa nawazuia watu wasiingie barabarani, nyote mnajua.

“Mwaka huu simzuii mtu, atakayeamua kufanya lolote kutetea haki yake, simzuii. Kwa hiyo, ngojeni muziki tarehe 27 na 28 mtauona,” amesema Maalim Seif.

“Tuiache demokrasia ifuate mkondo wake kwa amani. Tumekishwavumilia vya kutosha, sasa tunakwenda tarehe 27 na tarehe 28 tukiwa tayari kwa lolote lile litakalotokea. Kulinda demokrasia na kulinda haki ya Wazanzibari kumchagua rais wanayemtaka.”

Alisema, katika uchagzi wa mwaka huu, Wazanzibari hawawezi kuvumilia haki yao kuporwa na kwamba, tayari wameishapitia mengi katika maisha yao.

“Nataka kutahadharisha kuwa Wazanzibari wamedhamiria kulinda demokrasia kwa gharama yoyote, katu hatukubali kuendelea kudharauliwa. Wazanibari wameishapitia mengi, wamevuta subira na uvumilivu mkubwa na kupigiwa mfano. sasa imetosha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

error: Content is protected !!