Saturday , 3 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Ma RC, DC wapigwa ‘stop’ vituo kuhesabu, kutangaza matokeo  
Habari za Siasa

Ma RC, DC wapigwa ‘stop’ vituo kuhesabu, kutangaza matokeo  

Mwenyekiti wa NEC, Semistocles Kaijage
Spread the love

WAKUU wa Mikoa (RC) na Wilaya (DC) nchini Tanzania, ni miongoni mwa watendaji wa Serikali ambao hawatakiwi kuingia katika vituo vya kupiga, kuhesabu au kujumlishia kura. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Marufuku hiyo ipo katika Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2020 kilichotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) nchini Tanzania.

Sehemu ya tatu kifungu cha 3.3 ya kitabu cha maadili, imebainisha mambo manne yasiyotakiwa kufanywa na watendaji wa Serikali wakati wa uchaguzi utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

Mosi; mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kuchanganya ziara za kikazi na shughuli za kiuchaguzi na kutumia vyombo au watendaji wa Serikali katika shughuli za uchaguzi kwa manufaa yao.

Pili; mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya na viongozi wengine wa Serikali kuingia katika vituo vya kupigia, kuhesabu au kujumulishia kura.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dk. Wilson Mahera

Isipokuwa kwamba mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na viongozi wengine wa Serikali wanaruhusiwa kuingia katika kituo cha kupigia kura kwa madhumuni ya kupiga kura tu.

Kuhusu hilo, Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura wa NEC, Giveness Aswile amesema, maadili hayo yanapaswa kuzingatiwa na kila mmoja ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika na kumalizika salama.

Amesema, kama kuna mtu anakiuka maadili hayo mathalani wakuu hao wa mikoa na wilaya wataonekana katika chumba cha kuhesabu, kujumulisha na kutangaza matokeo wanaweza kukataa kwa kujaza fomu maalum ambazo zinakuwepo kulalamikia suala hilo.

Tatu; waziri au afisa mwandamizi yeyote wa Serikali kumwita msimamizi wa uchaguzi kwa lengo la kujadili masuala ya uchaguzi kuanzia kipindi cha kampeni mpaka kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi.

Nne; kuanzia kipindi cha kampeni za uchaguzi mpaka kutangazwa kwa matokeo, mawaziri hawaruhusiwi

I; kutangaza katika vyombo vya habari au kwa namna yoyote misaada au ahadi ya aina yoyote

II; kutoa ahadi za shughuli za maendeleo ya jamii kwa mfano, kujenga barabara, kusambaza maji na mambo mengine kama hayo kwa lengo la kuungwa mkono kisiasa

III; kutumia madaraka au rasilimali za Serikali kwa shughuli za kampeni za uchaguzi kwa manufaa ya chama chochote au mgombea yeyote.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!