Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu: Nilivyo si kama nilivyokuwa awali
Habari za Siasa

Lissu: Nilivyo si kama nilivyokuwa awali

Tundu Lissu akizungumza na wanahabari baada ya kutoka hospitali Nairobi
Spread the love

TUNDU Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amesema, anarejea nyumbani kwao Tanzania lakini alivyo sasa si kama alivyokuwa miaka mitatu iliyopita. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Lissu aliondoka nchini usiku wa tarehe 7 Septemba 2017 akiwa hajitambuia kupelekwa Hospitali Nairobi nchini Kenya akitokea Hospitali ya Rufaa Dodoma, Tanzania alipokuwa amepelekwa mchana wa siku hiyo baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana.

Mwanasiasa huyo alishambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 kati yake 16 zilimpata mwilini. Tangu wakati huo amekuwa akipata matibabu Nairobi kasha tarehe 6 Januari 2018 alihamishiwa nchini Ubelgiji kwa matibabu.

Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki akiwa na mkewe nchini Ubelgiji akifanya mazoezi

Tayari amekwisha kupona na kesho Jumatatu tarehe 27 Julai 2020 saa 7:20 mchana anarejea kwa ndege ya Shirika la Ndege la Emirates akitoa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.

Akizungumza na mtandao wa chombo cha habari cha Daily Nation leo Jiumapili tarehe 26 Julai 2020, akiwa kwenye maandalizi ya kurejea Tanzania, Lissu amesema, viungo vyake vina afya njema lakini havipo kama vilivyokuwa kabla ya kushambuliwa.

“Miguu yangu yote, kiuno changu, mikono yangu na tumbo langu vimeshambuliwa. Hivyo, kurudi katika hali ya kawaita itachukua muda mrefu,” amesema Lissu.

Tundu Lissu alipokuwa anasafirishwa kupoka Dodoma kwenda Nairobi

“Afya yangu ni nzuri kabisa ingawa sipo kama nilivyokuwa miaka mitatu iliyopita, lakini niseme nipo sawasawa. Ninajivuta vuta kidogo lakini ukiachana majeraha ya kushambuliwa, nipo vizuri.”

Kuhusu siasa za Tanzania na uchaguzi mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020 ambapo yeye ni miongoni mwa watia nia ya kugombea urais wa Tanzania ndani ya Chadema, amesema, tatizo kuba lipo kwenye uchaguzi huru na kuonesha mashaka baada ya upigaji kura kwenye uchaguzi huo.

Amesema, yapo matukio ambayo yamewafanya Watanzania kuwa waoga na kwamba, hilo ndio tatizo kubwa linaloikabili Tanzania kwa sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!