Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu: Chadema haijawahi kuridhiana na Serikali
Habari za Siasa

Lissu: Chadema haijawahi kuridhiana na Serikali

Spread the love

CHAMA Cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) kimeiomba Serikali ianze kutekeleza dhana ya maridhiano mapema kabla ya kubandika kwenye matangazo kuwa wameridhiana  kumbe si kweli. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro…(endelea).

Makamu Mwenyekiti CHADEMA Tundu Antipas Lissu alisema hayo jana tarehe 7 Mei 2023 wakati akizungumza na wakazi wa Morogoro Mjini ambapo aliwataka wananchi kushirikiana.

Amesema anashangaa kuona mabango yaliyoandikwa kwamba wameridhiana ilihali wao (Chadema) hawayajui na hawajawahi kufanya maridhiano.

Alisema maridhiano kwao ni nafasi pekee ya kuonesha wao walitaka nini na kinafanyika nini lakini kwa sasa hakuna hayo.

Alisema walishaandika mapendelezo ya maridhiano na kuyakabidhi lakini mpaka sasa hayajafanyiwa kazi.

“Tunachokiona kwa sasa ni picha zetu kuwemo kwenye mabango kuwa tumeridhiana, kivipi, wapi tumeridhiana, kuridhiana ni utekelezaji wa mapendekezo tuliyotoa na sio kuwekana kwenye picha ” alisema Lissu.

Akizungumzia katiba mpya Lisu alisema hadi kufikia mwaka wa uchaguzi 2025 ikiwa katiba mpya bado haijatoka hapatakalika.

Alisema katiba mpya ndio itasaidia kupata viongozi thabiti wataochaguliwa kupitia uchaguzi sahihi na wakiikosa ni wazi kwamba wataenda kwenye uchaguzi mgumu kama uliopitishwa mwaka 2020 ambapo wagombea wao walikatwa na kupitishwa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hivyo Lissu alliwataka wananchi kudai katiba mpya yenye mfumo mpya wa uchaguzi na haki zao.

Aidha, aliyewahi kugombea Ubunge Jimbo la Morogoro mjini CHADEMA, Devotha Minja

amewaomba wananchi  kushirikiana nae kwenda mahakama kuu kufungua kesi ya kudai viwanda sababu kwa vimejengwa kwa jasho la wananchi ambao ndio walipakodi na kufungwa kwake kunahatarisha maisha ya wakazi wa Morogoro ambao walivitegemea kwa ajili ya kujikimu.

“Miaka ya 1990 Morogoro ilikuwa ni vifijo na vigeregere kwa kufanya kazi kwenye viwanda, kulikuwa na viwanda vya kutosha ilikuwa huwezi kupata mdada  wala mkaka wa kazi lakini kwa sasa vijana wanapishana tu vijiweni, twende tukadai viwanda vyetu” alisema Minja.

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mlimba, Susan Kiwanga aliwataka wananchi wakiwemo wanawake kubadilika na kuipigia kura CHADEMA kwenye uchaguzi mkuu ujao ili waepukane na adha ya kulipia gharama za matibabu wakati wa kijifungua kwa kawaida au kwa upasuaji.

“Tangu mwaka 1960 CCM inasema huduma za mama na mtoto ni bure lakini mpaka sasa hakuna ukweli huo watu wanalipisha kila huduma wanayopewa sambamba na wanaofanyiwa upasuaji kulipishwa Sh 300,000, hiyo sahihi” alisema Kiwanga

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!