Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Ligi Kuu Tanzania Bara kurejea leo
Michezo

Ligi Kuu Tanzania Bara kurejea leo

Kikosi cha timu ya Namungo FC
Spread the love

 

LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), iliyokuwa imesimama kupisha kalenda ya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) ya michezo ya kirafiki kwa timu za Taifa, ligi hiyo inarejea tena kuanzia leo Jumanne, tarehe 15 Juni 2021. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo utakaopigwa leo Jumanne ni kati ya Biashara United dhidi ya Namungo FC, kuanzia saa 10:00 jioni, katika Uwanja wa Karume, mkoani Mara.

Ligi hiyo ilisimama kwa wiki mbili kupisha maandalizi ya kambi ya timu ya soka la Tanzania ‘Taifa Stars’ iliyocheza mchezo wa kirafiki na Malawi, juzi Jumapili, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam na kuibuka na ushindi wa 2-0.

Hadi ligi hiyo inasimama, mabingwa watetezi Simba ya Dar es Salaam, ilikuwa ikiongoza kwa pointi 67 baada ya kushuka dimbani mara 27 huku watani zao, Yanga wakishika nafasi ya pili ikiwa na pointi 61, baada ya kucheza michezo 29.

Mwadui FC inayoshika mkia kwenye msimamo wa ligi hiyo, ikiwa na pointi 19, baada ya kushuka dimbani mara 30, tayari imekwisha kata tiketi ya kushuka daraja.

Ushindani mwingine kwenye ligi hiyo inayoshirikisha timu 16, ni wanaowania ufungaji bora ambapo mshambuliaji wa Azam FC, Prince Dube, anaongoza kwenye mbio hizo, baada ya kuzifumania nyavu mara 14.

Anayefuati kwenye mbio hizo ni Nahodha wa Simba, John Bocco akiwa na magoli 13 na mshambuliaji mwenzake kwenye timu hiyo, Meddie Kagere akiwa na magoli 11.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!