Saturday , 10 June 2023
Home Kitengo Michezo Ligi Kuu Tanzania Bara kurejea leo
Michezo

Ligi Kuu Tanzania Bara kurejea leo

Kikosi cha timu ya Namungo FC
Spread the love

 

LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), iliyokuwa imesimama kupisha kalenda ya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) ya michezo ya kirafiki kwa timu za Taifa, ligi hiyo inarejea tena kuanzia leo Jumanne, tarehe 15 Juni 2021. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo utakaopigwa leo Jumanne ni kati ya Biashara United dhidi ya Namungo FC, kuanzia saa 10:00 jioni, katika Uwanja wa Karume, mkoani Mara.

Ligi hiyo ilisimama kwa wiki mbili kupisha maandalizi ya kambi ya timu ya soka la Tanzania ‘Taifa Stars’ iliyocheza mchezo wa kirafiki na Malawi, juzi Jumapili, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam na kuibuka na ushindi wa 2-0.

Hadi ligi hiyo inasimama, mabingwa watetezi Simba ya Dar es Salaam, ilikuwa ikiongoza kwa pointi 67 baada ya kushuka dimbani mara 27 huku watani zao, Yanga wakishika nafasi ya pili ikiwa na pointi 61, baada ya kucheza michezo 29.

Mwadui FC inayoshika mkia kwenye msimamo wa ligi hiyo, ikiwa na pointi 19, baada ya kushuka dimbani mara 30, tayari imekwisha kata tiketi ya kushuka daraja.

Ushindani mwingine kwenye ligi hiyo inayoshirikisha timu 16, ni wanaowania ufungaji bora ambapo mshambuliaji wa Azam FC, Prince Dube, anaongoza kwenye mbio hizo, baada ya kuzifumania nyavu mara 14.

Anayefuati kwenye mbio hizo ni Nahodha wa Simba, John Bocco akiwa na magoli 13 na mshambuliaji mwenzake kwenye timu hiyo, Meddie Kagere akiwa na magoli 11.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Benki ya NBC yakabidhi kombe la ubingwa wa ligi kuu kwa Yanga

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya...

HabariMichezo

Benki ya NBC yazindua kombe jipya la Ligi Kuu Tanzania Bara

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa Ligi ya NBC , Benki ya Taifa...

MichezoTangulizi

Yanga malizeni ugomvi na Fei Toto – Rais Samia

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

Michezo

Samia aipongeza klabu ya Yanga kwa hatua iliyofikia

Spread the love RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

error: Content is protected !!