Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo TFF yawatahadhalisha wanaotaka kuharibu uchaguzi
Michezo

TFF yawatahadhalisha wanaotaka kuharibu uchaguzi

Katibu Mkuu wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania, (TFF) Wilfred Kidao
Spread the love

 

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguuu Tanzania (TFF), limewataka wadau mbalimbali wa mchezo huo pamoja na wagombea waliojitokeza kwenye zoezi la uchukuaji fomu kwa ajili ya uchaguzi Mkuu kufuata taratibu na kanuni za uchaguzi ili kuondoa migogoro. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Rai hiyo imetolewa na katibu Mkuu wa Shirikisho hilo, Kidao Wilfred, kwenye makao makuu ya TFF, Karume Ilala Jijini Dar es Salaam.

Katibu huyo alitoa tahadhari kwa wadau wa mpira wa miguu kwa kuwataka, waiachie Kamati ya Uchaguzi ya TFF ifanye kazi yake mpaka zoezi hilo litakapoisha, bila kuwaingilia.

Aidha Kidao aliendelea kufunguka kuwa kama mchakato huo utaingiliwa basi kuna athari kubwa kama nchi, kupoteza vitu vingi kutoka kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), na Shirikisho la Mpira Duniani (FIFA), na kusisitiza kuwa kamati hiyo haitakiwi kuingiliwa na mtu yoyote kwa mujibu wa katiba ya TFF.

“Mchakato unaendeshwa kwa mujibu wa katiba ya TFF, sio Kidao wala Rais wa TFF anayepaswa kuingilia.

“Mchakato ukiingiliwa athari ya kwanza ni TFF kusimamishwa kwa uwanachama na Fifa, na timu za Taifa hazitaweza kushiriki mashindano ambayo yanaandaliwa na Caf pamoja na Fifa,” alisema Kidao

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!