Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari Ligi Kuu kuanza kutimua vumbi leo
HabariMichezo

Ligi Kuu kuanza kutimua vumbi leo

Spread the love

Ligi kuu ya soka Tanzania Bara msimu wa 2022/23 kuanza kutimua vumbi leo 15 Agosti 2022 kwa kushuhudia mechi mbili katika viwanja viwili tofauti ambapo Ihefu watakuwa wenyeji wa Ruvu Shooting huku Mtibwa Sugar akiwa mgeni wa Namungo katika ufunguzi huo wa Ligi . Anaripoti Damas Ndelema

Michezo wa kwanza utapigwa majira ya saa kumi kamili katika kiwanja cha Highland Estate uliopo mbeya  ambao ni uwanja wa nyumbani wa  klabu ya Ihefu ambayo imepanda daraja msimu huu ikitokea ligi daraja la kwanza ambapo katika mchezo huo watawakaribisha maafande wa Ruvu shooting  ya pwani na kila mmoja kutafuta alama tatu muhimu

Huku mchezo mwingine ukichezwa majira ya saa moja jioni ambapo Namungo watawakaribisha mtibwa Sugar katika dimba la Benjamin Mkapa ambao ndio utakuwa uwanja wao wa nyumbani mpaka pale uwanja wao wa Majaliwa  ambao upo kwenye marekebisho hivyo wataanza  harakati za kusaka ubigwa wa NBC leo dhidi ya wakata miwa hao wa Manungu katika dimba hilo la Benjamin Mkapa

Mashabiki wengi wa soka nchini walikua wakisubiri kwa hamu kurejea kwa Ligi kuu Tanzania Bara kutokana na usajili uliofanywa na timu zote katika dirisha hili la usajili huku ikitegemewa ligi hii itakuwa na ushindani mkubwa kutoka na sajili mbalimbali zilizofanywa kwani kuna wachezaji mbalimbali kutoka Afrika mpaka nje ya Bara hili la Afrika

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!