Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kusimamishwa uwakili; Fatma atuma ujumbe kwa JPM
Habari za SiasaTangulizi

Kusimamishwa uwakili; Fatma atuma ujumbe kwa JPM

Fatuma Karume, aliyekuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS)
Spread the love

WAKILI Fatma Karume amemueleza Rais John Magufuli kwamba, yuko tayari kukaa jela miaka 30, ili kuboresha demokrasia na utawala wa sheria nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Fatma ametoa kauli hiyo jana tarehe 20 Septemba 2019 kupitia ukurasa wake wa Twitter, saa kadhaa baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kumsimamisha uwakili kwa muda ikimtuhumu kutoa kauli za kuishambulia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

“Nimemalizika kwa kunifungia uwakili?Nyinyi mnaendeshwa kwa njaa ya matumbo yenu na si njaa ya haki! Mwambieni Rais Magufuli niko tayari kufa kwa Demokrasia na Utawala wa Sheria. Wasiojulikana wanajua nakaa wapi waje tu,” amesema Fatma.

Fatma aliyewahi kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) amesema kitendo cha kusimamishwa uwakili, hakitoshi kulipia thamani ya demokrasia na utawala wa sheria.

“Rais Magufuli nataka uelewe niko tayari kukaa jela miaka 30 kama kukaa kwangu jela italeta demokrasia na utawala wa sheria nchi hii.Kwa hivyo kuchukua haki yangu ya kusimamia sheria ni bei ndogo sana kulipia itikadi muhimu kama Demokrasia na utawala wa Sheria,” amesema Fatma

Jana, Mahakama Kuu iliamuru Fatma asiendelee kuwa wakili kwa muda, kutokana na upande wa serikali kulalamikia matamshi aliyotoa  katika kesi iliyofunguliwa na Ado Shaibu, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa ACT Wazalendo dhidi ya Rais Magufuli  na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!