Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea aikalia kooni Serikali Muswada wa Vyama vya Siasa
Habari za Siasa

Kubenea aikalia kooni Serikali Muswada wa Vyama vya Siasa

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Spread the love

MBUNGE  wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), katika jimbo la Ubungo, Saed Kubenea, amewavaa vigogo watatu ambao ni wanasheria nguli nchini kwa kupeleka muswaada wa sheria ya vyama vya siasa bungeni, wakati unavunja Katiba ya Nchi. Anaripoti Danson Kaijage kutoka Dodoma…(endelea).

Akizungumza bungeni jioni hii, Kubenea amesema, “muswada wa marekebisho wa vyama vya  siasa wa mwaka 2018, unavunja Katiba. Lakini muswaada huu, umeandaliwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi;  Mwasheria Mkuu wa Serikali (AG), Prof. Adelardus Kilangi na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mtungi.”

Alisema, “sisi tusio wanasheria tunaona vifungu vinavyopingana na sheria. Tuliwaambia kuwa rais atapoteza vyeo vyake kwenye muswada huu lakini wanachama wote wanaweza kupoteza uanachama lakini sio Rais.”

Amesema, muswaada huo haukupitia Baraza la Vyama vya Siasa na kwamba mwenyekiti wa baraza hilo, John Magale Shibuda, alimshukuru Spika wa Bunge, Job Ndugai, kuwaalika katika mjadala wa muswaada.

Kwa mujibu wa Kubenea, muswaada ulioletwa bungeni unamgeuza msajili wa vyama kuwa mlalamikaji, mwendesha mashitaka, jaji na bawana jela.

Kusikiliza mchango kamili wa Kubenea angalia video hapo chini

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!