Sunday , 23 June 2024
Home Habari Mchanganyiko Kivule walia barabara kujengwa kwa vifusi vya udongo badala ya changarawe
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kivule walia barabara kujengwa kwa vifusi vya udongo badala ya changarawe

Spread the love

WANANCHI wa Kata ya Kivule Mtaa wa Magole A, jijini Dar es Salaam, wameonesha kutoridhishwa na hatua ya barabara ya Nyang’andu kujengwa kwa kiwango cha udongo badala ya changarawe ili iweze kutumika katika nyakati zote. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Malalamiko hayo yameibuliwa leo tarehe 23 Mei 2024, siku chache baada ya barabara hiyo kumwagwa kifusi cha udongo, kinyume na maombi ya wananchi waliotaka kijengwe kwa changarawe wakati ikisubiri lami.

Akizungumza kwa niaba yao, Mwanaharakati huru, Bihimba Mpaya, amesema uamuzi huo hautasaidia kuwaondoa wananchi katika adha ya usafiri wanayoipata kutokana na barabara hiyo kuwa korofi hasa wakati wa mvua.

“Hii barabara badala ya kumwagwa kifusi cha changarawe chenye mawe wenyewe wanamwaga tope la udongo hapa umefanyika ufisadi mkubwa kupitia fedha za wananchi,” amesema Bihimba na kuongeza:

“Tunaiomba Serikali itekeleze maombi ya wananchi ili barabara hii ijengwe kwa changarawe ili iweze kupitika kwa muda wakati tunasubiri lami. Wakati wa mvua barabara haipitiki kabisa sasa Serikali imetoa pesa kuweka changarawe badala yake wameweka udongo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Askofu Wolfang Rais mpya TEC, Padri Kitima aula tena

Spread the loveBARAZA la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limetambulisha safu mpya za...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Washiriki mbio za NBC Dodoma Marathon kutumia treni ya SGR kwenda Dodoma

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

Habari MchanganyikoTangulizi

Padre anayetuhumiwa mauaji ya Asimwe, asimamishwa

Spread the loveKanisa Katoliki Jimbo la Bukoba limemsimamisha kutoa huduma za kichungaji...

Habari Mchanganyiko

Upandaji miti uzingatie kuondoa umaskini kwa wananchi

Spread the loveKATIBU Tawala wa mkoa wa Morogoro Dk. Musa Ally Musa...

error: Content is protected !!