Sunday , 16 June 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania, Msumbiji wajadili mikakati kuinua biashara, uwekezaji
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Tanzania, Msumbiji wajadili mikakati kuinua biashara, uwekezaji

Spread the love

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Msumbiji, Phaustine Kasike amekutana na Waziri wa Viwanda na Biashara wa Jamhuri ya Msumbiji, Silvino Augusto José Moreno na kukubaliana kufanikisha ushirikiano katika sekta ya biashara na uwekezaji kati ya nchi hizo mbili. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).


Pia katika mazungumzo hayo yaliyofanyika jana Jumatano kwenye Ofisi ya Wizara hiyo Jijini Maputo, viongozi hao wamekubaliana kutafuta mbinu na mikakati mahsusi ya kuongeza  kiwango cha biashara baina nchi hizi ili kiende sambamba na uhusiano wa kindugu, kihistoria na kijiografia baina ya nchi hizi.

Moja ya maeneo yaliyopendekezwa ni kuanzisha  Jukwaa la Pamoja la Biashara litakalowakutanisha wafanyabiashara na wadau wengine muhimu ili kubadilishana uzoefu, kujadili fursa mbalimbali za kiuchumi na kubaini namna ya kunufaika nazo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Rais Samia amng’oa Matinyi Maelezo, ateua viongozi mbalimbali

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali akiwamo...

Habari Mchanganyiko

DAWASA yaja na suluhisho la maji kwa wakazi wa Sinza C,D

Spread the loveWakazi wa Kata ya Sinza, Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar...

BiasharaHabari za Siasa

Tanesco yawasha mtambo namba 8 Bwawa Julius Nyerere

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Samia: Wakuu wa mikoa, wilaya wanaendeleza ubabe

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema bado wakuu wa wilaya na...

error: Content is protected !!