Tuesday , 3 October 2023
Home Habari Mchanganyiko Kitilya na wenzake sasa huru, wakamatwa tena
Habari Mchanganyiko

Kitilya na wenzake sasa huru, wakamatwa tena

Spread the love

BAADA ya kusota mahabusu ya Magereza kwa miaka mitatu, aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitiyla na wenzake, hatimaye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru leo tarehe 11 Januari, 2019. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Watuhumiwa wengine katika kesi hiyo ni Shose Sinara, Mkuu wa Idara ya Uwekezaji wa Benki ya Stanbic na Sioi Solomon, Mwanasheria wa Stanbic Tanzania.

Leo Mbele ya Hakimu Mkazi, Salum Ally watuhumia hao aliwachiwa huru baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka kutokuwa na nia ya kuendelea na kesi hiyo kama alivyopewa mamlaka na kifungu cha 91 (1) cha Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA).

Wakili wa Selikali, Hashim Ngole aliieleza mahakama hiyo kuwa DDP ameamua kutoendelea na shtaka hilo.

Hakimu Ally aliamua kuwaacha huru watuhumiwa hao.

Watuhumiwa hao walipandishwa kizimbani katika mahakama hiyo kwa kosa la kuhujumu uchumi wakidaiwa kughushi nyaraka na kufanikisha uhalifu huo kati Agosti 2012 na Machi 2013 jijini Dar es Salaam.

Kosa la pili, linadaiwa kufanywa na Sinare, tarehe 2 Agosti mwaka 2012 kwa kughushi hati ya mkopo wa Dola za Marekani 550 milioni katika Benki ya Stanbic ya Tanzania na Benki ya Standard ya Uingereza akiiombea fedha Serikali ya Tanzania.

Sinare anatuhumiwa kwa kosa la tatu alilotenda tarehe 13 Agosti 2012, la kupeleka hati ya kughushi kwenye Wizara ya Fedha iliyoonesha kuwa Serikali ya Tanzania itapewa mkopo wa Dola za Marekani 550 milioni kutoka Benki ya Stanbic ya Tanzania na Standard ya Uingereza.

Washitakiwa hao pia wote wanakabiliwa na kosa la kutengeneza mkataba bandia tarehe 5 Novemba, mwaka 2012 jijini Dar es Salaam katika Makao Makuu ya Benki ya Stanbic kupitia Kampuni ya Enterprise Growth Market Advisor (EGM).

Shitaka lingine linalowakabili watuhumiwa wote ni utakatishaji fedha wanalodaiwa kulitenda kati ya mwezi Machi 2013 na Septemba 2015.

Washitaki2a hao baada ya kuachiwa huru na mahakama, Polisi wamewakama tena.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia

Spread the loveJESHI la Polisi mkoani Songwe limewakamata watu wawili kwa tuhuza...

AfyaHabari Mchanganyiko

Chanjo mpya ya malaria Sh 5,000-10,000

Spread the loveShirika la afya la Duniani (WHO) limeridhia chanjo ya pili...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wagonjwa kiharusi waongezeka, Hospitali Mkapa yaja matibabu mapya

Spread the loveHOSPITALI ya Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na madaktari Bingwa kutoka...

Habari Mchanganyiko

Wananchi waamua kujenga zahanati kukwepa adha kufuata huduma mbali

Spread the loveWANANCHI wa Kijiji cha Kwikerege, kilichopo katika Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!