MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, amesema wasiokitakia mema chama hicho wanawatoa kwenye ajenda muhimu na kujikuta wakijadili mambo yasihusu ajenda za wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Kinana ameyasema hayo leo Jumapili tarehe 27, Novemba, 2022, wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 10 wa Jumuiya ya Vijana UVCCM, jijini Dodoma.
“Wasio tutakia mema huwa wanatutoa kwenye ajenda muhimu na sisi kwasababu hatujiandaa tunafuata mkumbo na kuanza kujadili mambo ambayo hayana uhusiano wa moja kwa moja na mambo ambayo tumeahidi Watanzania, amesema Kinana.
Amesema kazi mojawapo ya jumuiya ya chama hicho ni kusemea na kutetea chama na Serikali za pande zote za muungano kwa kutumia hoja nzuri ambapo amewataka vijana kusoma ili kupata hoja za kusema na kutetea.
“Hoja hushindwa na hoja bora zaidi na hoja iliyobora zaidi haitoki hewani, haiwezi kubuniwa lazima iwe ni hoja iliyofanyiwa uchambuzi. Wakati mwingine nasoma watu wanavyobishana na huoni uzito mkubwa sana wa mabishano au thamani ya hoja zinazobishaniwa,” amesema Kinana
Katika hatua nyingine Kinana amesema ni uykweli kwamba ndani ya Seriklai ya awamu ya sita fedha nyingi za maendeleo zimepelekwa kwa wananchi na kufanya kazi kuliko kipindi kingine chochote.
“Tangu nimekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hiki, nimetembelea mikoa 12… jambo moja ambalo limekuwa dhahiri kwamba fedha nyingi zimetolewa na kazi zimefanyika. Hakuna kipindi ambacho fedha nyingi za maendeleo zimetolewa kama hivi sasa hatusemi kwa kusifia bali huo ndio ukweli wenyewe,” amesema.
Hakuna uwazi wa matumizi ya hizo fedha kwa minajiri ya thamani ya mradi. Value for money + impact kwa wananchi wanaolengwa.