JAKAYA Mrisho Kikwete, Rais mstaafu wa Tanzania amesema, atafurahia iwapo Yanga itaibuka na ushindi dhidi ya mtani wake, Simba. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Kikwete ametoa kauli hiyo leo Jumapili, tarehe 27 Juni 2021, katika mkutano mkuu wa klabu hiyo uliofanyika ukumbi wa DYCC-Temeke, mkoani Dar es Salaam.
Yanga na Simba, zitacheza mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara, tarehe 3 Julai 2021, saa 11 jioni, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
Kikwete ambaye ni shabiki wa mabingwa hao wa kihistoria amesema “Yanga naipenda, inapofanya vizuri nafurahi sana na inapofanya vibaya nasononeka na matumaini yangu Jumamosi ijayo itafanya vizuri.”
Pia, watani hao wa jadi, watakutana tarehe 25 Julai 2021, katika Uwanja wa Tanganyika, mkoani Kigoma kwenye fainali ya Kombe la Azam Sports Federetion Cup (ASFC).
Leave a comment