Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kifo cha Kaunda: Tanzania yatangaza siku 7 za maombolezi
Habari MchanganyikoKimataifa

Kifo cha Kaunda: Tanzania yatangaza siku 7 za maombolezi

Bendera ya Tanzania ikiwa nusu mlingoti ikiadhimisha maombelezo
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametangaza siku saba za maombolezo ya kitaifa kufuatia kifo cha Rais wa kwanza wa Zambia, Kenneth Kaunda. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kaunda (97), alifikwa na mauti jana Alhamisi, tarehe 17 Juni, 2021 mjini Lusaka Zambia.

Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa na Jaffar Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu imesema, katika kipindi hicho cha maombolezo, bendera zote zitapepea nusu mlingoti.

Aidha, Rais Samia ametuma salamu za rambirambi kwa Rais wa Zambia, Edgar Chagwa Lungu, familia ya marehemu na wananchi wote wa Zambia kwa kumpoteza kiongozi wao.

Hayati Kenneth Kaunda

Rais Samia amemtaja Hayati Kaunda kuwa miongoni mwa viongozi mahiri na jasiri kuwahi kutokea barani Afrika.

Wakati wa uhai wake, alitoa mchango mkubwa kwenye harakati za ukombozi wa Bara la Afrika kwa kushirikiana na viongozi wengine, akiwemo Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Vilevile, Hayati Kaunda alikuwa miongoni mwa waanzilishi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan

Tanzania itamkumbuka Hayati Kaunda kwa mchango wake katika kukuza uhusiano na ushirikiano kati ya mataifa yetu mawili, ambao uliwezesha kutekelezwa kwa miradi mikubwa ya kimkakati, ikiwemo Mamlaka ya Reli kati ya Tanzania na Zambia (Tazara) na Bomba la Kusafirisha Mafuta (Tazama).

Hayati Kaunda, alikuwa Rais wa Zambia kwa miaka 27 kuanzia tarehe 24 Oktoba 1964 hadi 2 Novemba 1991.

Alizaliwa tarehe 28 Aprili 1924.

Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema Peponi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!