Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kesi ya Sabaya na wenzake yaiva, kuanza kujitetea kesho
Habari MchanganyikoTangulizi

Kesi ya Sabaya na wenzake yaiva, kuanza kujitetea kesho

Spread the love

 

ALIYEKUWA Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili, wamekutwa na kesi ya kujibu katika mshtaka ya unyang’anyi wa kutumia silaha, yanayowakabili kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Odira Amworo, imemkuta Sabaya na wenzake, Sylvester Nyegu na Daniel Mbura, wana kesi ya kujibu, leo Alhamisi, tarehe 12 Agosti 2021, baada ya mashahidi upande wa Jamhuri kutoa ushahidi wao mahakamani hapo.

Hivyo, imepanga kuanza kusikiliza utetezi wa washtakiwa hao kesho Ijumaa, tarehe 13 Agosti mwaka huu.

Sabaya na wenzake wanakabiliwa na mashtaka matatu katika kesi hiyo iliyofunguliwa mahakamani hapo Juni 2021, ambapo wanadaiwa kutenda makosa hayo tarehe 9 Februari 2021, kwenye duka la Mohamed Saad, lililoko eneo la Bondeni jijini Arusha.

Kwa mara ya kwanza, Sabaya na wenzake walifikishwa kizimbani tarehe 4 Juni 2021 na kusomewa mashtaka hayo.
Katika kesi hiyo, washtakiwa hao wanadaiwa kumfanyia unyang’anyi wa kutumia silaha, Diwani wa Sombetini (CCM), Bakari Msangi na kumuibia Sh. 390,000.

Pia, washtakiwa hao wanadaiwa kumpiga mateke na kumtishia silaha, Ramadhani Ayoub, kisha kumpora simu na Sh. 35,0000.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!