Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Sh. 2.9 Tril. kufanya mageuzi mtandao wa barabara Tanzania
Habari Mchanganyiko

Sh. 2.9 Tril. kufanya mageuzi mtandao wa barabara Tanzania

Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Ummy Mwalimu
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imepanga kutumia Sh. 2.974 trilioni, kwa ajili kuongeza mtandao wa barabara za lami na changarawe, pamoja na ujenzi wa madaraja, katika kipindi cha miaka mitano (2021/22 hadi 2025/26). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Alhamisi, tarehge 12 Agosti 2021 na Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Ummy Mwalimu, akifungua mkutano wa wizara hiyo na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tarura), uliofanyika jijini Dodoma.

Ummy amesema, katika kipindi hicho cha miaka mitano, Serikali kupitia Tarura, itajenga barabara za kiwango cha lami zaidi ya kilomita 1,000, za changarawe kilomita 73,242 na madaraja 3,808.

“Serikali kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2021/22 hadi 2025/26, imepanga kuongeza mtandao wa barabara za lami kutoka kilometa 2,404.90 hadi kilometa 3,855.65, changarawe kutoka kilometa 29,116.57 hadi kilomita 102,358.14 na madaraja toka 2,812 hadi 6,620,”

“Fedha zitakazotumika kwenye mpango huu zinakadiriwa kuwa Shilingi trilioni 2.974,” amesema Ummy.

Ummy ameiagiza Tarura kufuata vigezo stahiki katika utekelezaji mpango huo, ikiwemo kuzingatia usawa katika ugawaji wa rasilimali fedha za ujenzi wa miundombinu hiyo.

“Aidha, fursa za kiuchumi na kijamii zipewe umuhimu, ili kuweza kuongeza mtandao wa barabara katika maeneo ya vijijini,” amesema Ummy.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!