Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Kesi ya dhamana ya Sudi Brown, Maua Sama, Shaffih kusikilizwa J’tatu
Habari Mchanganyiko

Kesi ya dhamana ya Sudi Brown, Maua Sama, Shaffih kusikilizwa J’tatu

Spread the love

KESI ya maombi ya dhamana Na. 13/2018 ya Msanii wa Bongo Fleva, Maua Sama, Watangazaji Sudi Kadio maarufu kama Soudy Brown na Shaffih Dauda na wengine wanne kuanza kusikilizwa siku ya Jumatatu tarehe 24 Septemba 2018. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Kwa mujibu wa Wakili Jebra Kambole, kesi hiyo dhidi ya Mkuu wa Jeshi la Polsi, Mkurugenzi wa Uplelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) na wengine itasikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi, Huruma Shahidi.

Maua Sama na Soudy Brown wanashikiliwa na Jeshi la Polisi katika Kituo cha Polisi cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam tangu Jumapili ya tarehe 16 Septemba mwaka huu, kwa tuhuma za kudhalilisha fedha ya Tanzania.

Wakati Mtangazaji Shafii Dauda, Anthony Luvanda (MC Luvanda), Michael Mlingwa, Fadhili Kondo na Benedict Felix Kadege wakishikiliwa kwa tuhuma za kuendesha mtandao wa Youtube pasipo kusajili katika Mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA).

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!