SERIKALI imesema itagharamia shughuli za mazishi ya miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali ya MV Nyerere iliyotokea juzi tarehe 20 Septemba 2018. Anaripoti Regina Kelvin…(endelea).
Hayo yalisemwa jana tarehe 21 Septemba 2018 na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwele wakati akizungumza na wanahabari kisiwani Ukerewe mkoani Mwanza.
Mhandisi Kamwele amesema utaratibu wa mazishi ikiwemo eneo la mazishi utatolewa baadae na serikali.
Kivuko cha MV Nyerere kilizama katika Ziwa Victori kikitokea Bugorora kisiwani Ukerewe kuelekea Kisiwa cha Ukara.
Leave a comment