Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Juma Duni Haji aikosoa SMZ
Habari za Siasa

Juma Duni Haji aikosoa SMZ

Spread the love

CHAMA cha ACT-Wazalendo kimedai kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), ina tabia ya kutenga bajeti isiyokidhi mahitaji pia kukopa kwa masharti magumu na riba kubwa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari hivi karibuni visiwani Zanzibar, Naibu Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Juma Duni Haji amesema Sh. 400 Bilioni zilizotengwa katika mwaka wa fedha wa 2019/20, hazikidhi mahitaji ya kiuchumi na ustawi wa jamii ya visiwa hivyo.

Duni ameeleza kuwa, Visiwa vya Zanzibar vina changamoto nyingi hususan katika sekta ya afya, elimu, miundombinu na maji.

“Nimeelezwa kwamba, bajeti hiyo itakuwa na nakisi ndogo ya 400 Bilioni, kwa kweli bajeti hii ni ndogo sana ukilinganisha na mahitaji ya kiuchumi na ustawi wa jamii ya Zanzibar,” amesema Duni.

Wakati huo huo, Duni amesema kitendo cha SMZ kukopa madeni yenye riba kubwa na masharti magumu, kimepelekea serikali hiyo kuwa na malimbikizo ya madeni ya ndani na nje ya nchi.

Amesema, hadi sasa Zanzibar inadaiwa Sh. 815.9 Bilioni, huku deni la nje likiwa ni Sh. 678.4 Bilioni na kwamba, SMZ imeshindwa kulipa kwa wakati malimbikizo ya viinua mgongo vya wastaafu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!