Friday , 2 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Juma Duni Haji aikosoa SMZ
Habari za Siasa

Juma Duni Haji aikosoa SMZ

Spread the love

CHAMA cha ACT-Wazalendo kimedai kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), ina tabia ya kutenga bajeti isiyokidhi mahitaji pia kukopa kwa masharti magumu na riba kubwa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari hivi karibuni visiwani Zanzibar, Naibu Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Juma Duni Haji amesema Sh. 400 Bilioni zilizotengwa katika mwaka wa fedha wa 2019/20, hazikidhi mahitaji ya kiuchumi na ustawi wa jamii ya visiwa hivyo.

Duni ameeleza kuwa, Visiwa vya Zanzibar vina changamoto nyingi hususan katika sekta ya afya, elimu, miundombinu na maji.

“Nimeelezwa kwamba, bajeti hiyo itakuwa na nakisi ndogo ya 400 Bilioni, kwa kweli bajeti hii ni ndogo sana ukilinganisha na mahitaji ya kiuchumi na ustawi wa jamii ya Zanzibar,” amesema Duni.

Wakati huo huo, Duni amesema kitendo cha SMZ kukopa madeni yenye riba kubwa na masharti magumu, kimepelekea serikali hiyo kuwa na malimbikizo ya madeni ya ndani na nje ya nchi.

Amesema, hadi sasa Zanzibar inadaiwa Sh. 815.9 Bilioni, huku deni la nje likiwa ni Sh. 678.4 Bilioni na kwamba, SMZ imeshindwa kulipa kwa wakati malimbikizo ya viinua mgongo vya wastaafu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!