JUKWAA la Katiba Tanzania (JUKATA), limeiomba Serikali kutoa ratiba ya utekelezaji wa marekebisho ya Sheria na namna ya kukwamua mchakato wa upatikanaji katiba mpya, ili kuruhusu ushiriki mpana wa wadau na wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Wito huo umetolewa leo Jumatano, tarehe 4 Januari 2022 na Mkurugenzi Mtendaji na Katibu wa Bodi wa JUKATA, Bob Wangwe, siku Moja baada ya Rais Samia Suluhu Hassan, kusema Serikali yake Iko tayari kukwamu mchakato wa marekebisho ya katiba uliokwama 2014.
“JUKATA tunaisihi Serikali kutoa ratiba ya utekelezwaji wa marekebisho ya Sheria na namna ya kukwamua mchakato wa katiba moya Ili kuruhusu ushiriki Mpana wa wadau na wananchi kwenye michakato hiyo,” imesema taarifa ya Wangwe.
Aidha, Wangwe amesema JUKATA iko tayari kutoa ushirikiano na usaidizi wa kitaalamu katika kuhakikisha utekelezaji wa michakato hiyo inafanikiwa kwa lengo la kujenga demokrasia.
Katika hatua nyingine, JUKATA imempongeza Rais Samia kwa kuondoa zuio la mikutano ya hadhara, kufanya marekebisho ya Sheria na utayari wake wa kukwamua mchakato wa katiba.
Leave a comment