Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko JUKATA yataka ratiba mchakato marekebisho ya sheria, katiba mpya
Habari Mchanganyiko

JUKATA yataka ratiba mchakato marekebisho ya sheria, katiba mpya

Spread the love

JUKWAA la Katiba Tanzania (JUKATA), limeiomba Serikali kutoa ratiba ya utekelezaji wa marekebisho ya Sheria na namna ya kukwamua mchakato wa upatikanaji katiba mpya, ili kuruhusu ushiriki mpana wa wadau na wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Wito huo umetolewa leo Jumatano, tarehe 4 Januari 2022 na Mkurugenzi Mtendaji na Katibu wa Bodi wa JUKATA, Bob Wangwe, siku Moja baada ya Rais Samia Suluhu Hassan, kusema Serikali yake Iko tayari kukwamu mchakato wa marekebisho ya katiba uliokwama 2014.

“JUKATA tunaisihi Serikali kutoa ratiba ya utekelezwaji wa marekebisho ya Sheria na namna ya kukwamua mchakato wa katiba moya Ili kuruhusu ushiriki Mpana wa wadau na wananchi kwenye michakato hiyo,” imesema taarifa ya Wangwe.

Aidha, Wangwe amesema JUKATA iko tayari kutoa ushirikiano na usaidizi wa kitaalamu katika kuhakikisha utekelezaji wa michakato hiyo inafanikiwa kwa lengo la kujenga demokrasia.

Katika hatua nyingine, JUKATA imempongeza Rais Samia kwa kuondoa zuio la  mikutano ya hadhara, kufanya marekebisho ya Sheria na utayari wake wa kukwamua mchakato wa katiba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!