Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM: Sitaki kisingizio cha corona
Habari za Siasa

JPM: Sitaki kisingizio cha corona

Spread the love

 

RAIS John Magufuli ametaka miradi mbalimbali nchini kukamilika kwa wakati, na kwamba hataki kusikia imesimama kwa sababu ya corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Amesema, miradi ya barabara ya njia nane kutoka Dar es Salaam kwenda Kibaha inaendelea kujengwa, Daraja la Kijazi (Ubunge) limejengwa na mingine haijasimama, hivyo amewataka viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaokagua miradi, wasisikilize kwamba imeshindwa kukamilika kutokana na corona.

“… hatutaki visingizio, niwatake watendaji wangu pasiwe na kisingizio chochote cha ugonjwa wa corona wanapokagua miradi,” ametoa kauli hiyo leo tarehe 24 Februari 2021 katika uzinduzi wa Daraja la Juu la Kijazi, Ubungo jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia ujenzi wa daraja hilo, amewashukuru wakandarasi kwa kumaliza mradi huo kwa wakati, na kwamba wakandarasi wengine nao wamalize kazi kwa wakati.

“Nitoe wito kwa makandarasi wengine nchi nzima, wasitafute visingizio vya kuchelewa kazi, mara corona mara sijui nini. Hawa wamemaliza na corona ilikuwepo na daraja limekamilika.

“Mara wataalamu wetu wapo nje, vifaa haviingii kwa sababu ya corona, ni wizi unaofanywa na makandarasi na ndiyo maana mnaona daraja hili limekamilika na corona ipo,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!