Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko JPM atumia staili ya China kuikabili corona, wagonjwa wafika 12
Habari Mchanganyiko

JPM atumia staili ya China kuikabili corona, wagonjwa wafika 12

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli ameagiza, wageni wote watakaoingia nchini, wawekwe karantini kwa siku 14 kwa gharama zao. Anaandika Hamis Mguta,Dar es Salaam…(endelea).

kwa sasa, China inaruhusu wageni kutoka mataifa mbalimbali kuingia nchini humo kwa sharti la kuwekwa karantini kwa siku 14, ili kujiridhisha kama mgeni huyo hajaambukizwa. kwa siku zote 14, gharama ni za mgeni.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 22 Machi 2020, alipohudhuria ibada ya Jumapili katika Kanisa la Mtakatifu Paul wa Msalaba, Jimbo Kuu la Katoliki Dodoma iliyoongozwa na paroko wa parokia hiyo Onesmo Wisi.

Pia amewataka Watanzania kutotishwa na ugonjwa huo, na badala yake waendelee kuchapa kazi na kujenga uchumi huku wakizingatia tahadhari zote za kujikinga kuambukizwa ugonjwa huo kama zilivyotolewa na Wizara ya Afya.

Katika salamu zake katika Ibada hiyo, Magufuli amesema kuwepo kwa ugonjwa wa corona isiwe sababu ya kutishana kiasi cha kumsahau Mungu.

Ametoa wito kwa Wakristo na waumini wa madhehebu mengine kumrudia Mungu ili aepusha janga hili, badala ya kumwacha shetani atawale.

Kiongozi mkuu huyo wa nchi amekemea tabia za baadhi ya watu wanaofanya mzaha juu ya ugonjwa huu ama kuwatia hofu wananchi kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, na badala yake ametaka Watanzania waendelee kuchapa kazi huku wakizingatia tahadhari.

“Watu tusitishane, tunatishana mno. Niwaombe ndugu Wakristo na Watanzania kwa ujumla wa madhehebu yote, huu ndio wakati mzuri sana wa kumtegemea Mungu kuliko wakati wote,.”

“Tuendelee kuchapa kazi, tuendelee kuujenga uchumi wetu, hatuwezi kusalimu amri kwa ugonjwa huu wa Corona na kushindwa kumtegemea Mungu na tukashindwa kuendeleza uchumi wetu,” amesema Magufuli.

Amewashukuru viongozi wa Dini kwa kuungana na Serikali katika kuwahamasisha wananchi kuchukua tahadhari na ametoa wito kwa viongozi hao kuendelea kuliombea Taifa ili Mungu aepushe ugonjwa huo uliosababisha vifo vya watu zaidi ya 13,000 duniani kote hadi jana saa 5 usiku.

Hadi sasa rais Magufuli amesema kuna wagonjwa 12 waliothibitika kuwa na ugonjwa wa Corona lakini wanaendelea vizuri na kuwa mgonjwa wa kwanza aliyegundulika na ugonjwa huo nchini amepona.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!