Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM ‘aitekenya’ Chadema
Habari za Siasa

JPM ‘aitekenya’ Chadema

Spread the love

USHAURI wa Rais John Magufuli, uliyomtaka Biswalo Maganga, Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DPP), kuangalia namna ya kuzungumza na watuhumiwa wa uhujumu uchumi na kuwaacha huru, imejibiwa vikali na Chadema. Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Chama hicho kimeeleza kushtushwa na kauli hiyo, huku kikidai ushauri huo unatokana baadhi ya watuhumiwa kushikiliwa kwa makosa.

Tarehe tarehe 22 Septemba 2019, Rais Magufuli alimshauri Maganga, kwa kuzingatia sheria, kuangalia uwezekano wa kushughulika na watuhumiwa hao kama wapo tayari kurejesha fedha, basi wafanye hivyo.

Leo tarehe 24 Septemba 2019 kupitia tamko lao, Chadema kimedai, ushauri huo unatokana na ‘kusutwa’ na dhamira kwamba, baadhi ya waliokamatwa, walionewa.

Tamko la Chadema lililotolewa na Tumaini Makene, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama hicho limeeleza, watuhumiwa hao wanastahili uhuru.

“…si tu imethibitisha madai ya kuwepo uonevu katika kile kilichoitwa vita dhidi ya ufisadi, bali pia inadhihirisha kuwa watuhumiwa hao wanastahili haki, uhuru wao bila masharti na waombwe samahani, badala ya wao kuomba,” limeeleza tamko hilo.  

Tamko hilo limeeleza kwamba, mpaka sasa baadhi ya makosa ya watuhumiwa yameshindwa kuthibitishwa hivyo kusababisha kuendelea kuwa mahabusu kwa muda mrefu.

Chama hicho kimeeleza, kwa muda mrefu makundi mbalimbali yamekuwa yakilalama namna vita ya ufisadi kutowatendea haki baadhi ya watu.

“Hii inathibitisha kauli na madai ya watu na makundi mbalimbali katika jamii, ikiwemo Chadema yenyewe, ambayo mara kadhaa kupitia majukwaa mbalimbali, imetoa kauli kuwa vita iliyokuwa inaendeshwa na serikali, ililenga kuwaonea baadhi ya watu,” imedai sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imeeleza wasiwasi kwamba, mpaka sasa baadhi ya watuhumiwa, hawajathibitishwa kuhusika na tuhuma hizo na kuhoji “watawezaje kukiri kuhusika kwenye tuhuma hizo?”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!